Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya vifaa vya kufundishia na uhaba wa Wakufunzi katika Chuo cha Afya kilichopo Hospitali ya Kitete?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Kwanza ninasikitika sana kwa majibu ya Serikali ya jumla namna hii, kwa sababu mpaka naleta swali hili tayari nilikuwa nafahamu kwamba kuna mapungufu ya Wakufunzi pamoja na vifaa vya kufundishia. Wakati wanafunzi wakiwa 24 ndiyo fedha zilipelekwa, leo kuna wanafunzi zaidi ya 280 hakuna walimu, walimu ni hao unaowasema hawa 11 hao wakufunzi ndiyo waliyopo. Ninaomba nipate commitment ya Serikali, ni lini mtapeleka wakufunzi ili chuo hichi kiweze kufanya vizuri kama vilivyo vyuo vingine? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, hizi Maabara zinafanyiwa ukarabati lakini mpaka sasa hata vifaa vya kufundishia kwenye hizi Maabara bado hazijaenda Mheshimiwa Naibu Waziri. Hebu naomba mnipe majibu halisi watu wa Tabora wasikie, ni lini mtapeleka fedha ili vifaa vipelekwe na wanafunzi hawa waweze kupata mafunzo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kukipenda chuo chake. Pamoja na swali lake hili Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini aliandika barua, nimuombe sasa specifically mimi na yeye tukishamaliza hapa, tukishamaliza leo Bunge hili na tukamaliza bajeti yetu, tuende mimi pamoja na yeye akathibitishe hivi vyote ambavyo nimemwambia hapa.

Tutakwenda mimi na wewe, najua ulikwenda ukakuta hayo matatizo na hukurudi tena, baada ya wewe kuuliza hili swali Mheshimiwa Waziri wa Afya alielekeza na kazi imefanyika. Twende pamoja ili usimamie hizi fedha ambazo zimeshapelekwa uhakikishe zimefanya kazi ambayo wewe ulitegemea. (Makofi)