Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 202 2022-05-16

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya vifaa vya kufundishia na uhaba wa Wakufunzi katika Chuo cha Afya kilichopo Hospitali ya Kitete?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya vifaa vya kufundishia katika Chuo cha Afya Tabora na tayari imepeleka vifaa vyenye thamani ya Shilingi Milioni 115.7 kwa ajili ya kuboresha mafunzo kwenye chuo hicho. Pamoja na ununuzi wa vifaa hivyo, Serikali imepeleka Shilingi Milioni 267.8 kwa ajili ya ukarabati wa maabara Nne za kufundishia. Aidha, mpaka sasa Serikali imepeleka watumishi 11 wanaofundisha chuoni hapo ili kupunguza upungufu wa wakufunzi. Ahsante.