Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED aliuliza: - Je, Shirika la Ndege nchini (ATCL) limeshaanza kulipa madeni ya Makampuni yaliyokuwa yanatoa huduma?

Supplementary Question 1

MHE. ALI JUMA MOHAMED: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza hivi sasa shirika letu la Ndege Tanzania limeanza safari zake za kubeba mizigo kwa ajili ya safari Guangzhou China, inaondoka China na kupitia Zanzibar na baadaye inarudi Zanzibar. Shirika hivi sasa wanatumia ndege yake ya Boeing 787 kwa ajili ya kubeba mizigo hiyo. Ndege hii imeundwa kwa ajili ya kubeba abiria na mizigo lakini eneo kubwa ya ndege hii ni kwa ajili ya kubeba abiria. Shirika letu sasa linabeba mizigo bila ya abiria kwa kwenda huko China.

Je, Shirika halioni hivi sasa kuendelea kufanya hivyo ni kuendelea kulitia hasara?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, hivi sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la abiria kati ya Zanzibar, Pemba na Dar es Salaam. Je, ni lini Shirika la Ndege la Air Tanzania litaanza safari zake katika Kisiwa cha Pemba? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ali Juma Mohamed Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna Ndege aina ya Dreamliner 787-8 ambayo inafanya biashara kati ya Tanzania na China na Ndege hii imekuwa ikibeba abiria lakini kipindi cha Covid 19 China kama tunavyofahamu kuingia abiria yeyote ndani ya nchi ya China. Kwa hiyo tukaona ni heri na bora Ndege hii aina ya 787-8 Dreamliner ambayo ina uwezo wa kubeba tani 40 ifanye biashara ya kubeba mizigo kuliko tungeiacha kuwa grounded na ingekuwa gharama zaidi kuliko hivi sasa ambavyo ipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge anatamani ama anapenda kwamba tuanzishe safari za kwenda Pemba. Nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote wa Zanzibar kwamba Shirika letu la ATCL litaanza safari zake za Pemba mwaka wa fedha 2023/2024 kwa maana ya kwamba mwaka ujao, ahsante. (Makofi)