Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 206 2022-05-16

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED aliuliza: -

Je, Shirika la Ndege nchini (ATCL) limeshaanza kulipa madeni ya Makampuni yaliyokuwa yanatoa huduma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Juma Mohamed Mbunge wa Shaurimoyo kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kulipa madeni ya makapuni yanayotoa ama yaliyokwisha kutoka huduma kwa ATCL baada ya kuyafanyia uhakiki. Mwaka 2016 kabla ya Serikali kuanza mpango wa kuifufua ATCL Kampuni ilikuwa inadaiwa kiasi cha shilingi bilioni 141.77 na watoa huduma mbalimbali wa ndani na nje. Hadi kufikia mwezi Aprili, 2022 Serikali imelipa madeni jumla ya shilingi bilioni 127.07.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuiwezesha ATCL kulipa madeni yaliyobaki kulingana na uwezo wa kibajeti. Ahsante.