Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Nina swali moja tu la nyongeza. Kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali kwa sababu mradi huu umeanza muda mrefu sana. Wilaya yetu ya Chemba miji yake mingi ipo pembezoni na ni ukweli kwamba eneo la mjini lina watu wachache sana. Sasa nataka kujua nini mpango wa Serikali wa kupeleka hii huduma ya Vituo vya Polisi kwenye miji hiyo mikubwa? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Wilaya ya Chemba sehemu kubwa ni Wilaya ya Vijijini na ina miji inayozunguka mji wenyewe wa Chemba, pale panahitajika pia utaratibu wa kuimarisha ulinzi kwenye maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimwahidi tu Mheshimiwa Monni kwamba tulikubaliana nitafanya ziara, moja ya lengo ni kuangalia maendeleo ya ujenzi huu, lakini la pili ni kuangalia maeneo ambayo kimkakati yanastahili kupewa huduma za kipolisi ili kuimarisha usalama wa raia na mali zao. Tutakapofika huko Mheshimiwa tutakubaliana ni maeneo gani yapewe kipaumbele. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Wananchi wa Kishapu, Mfuko wa Jimbo wa Mbunge wa Jimbo la Kishapu, lakini pia na wadau wa maendeleo kama Mwadui na wengine wameweza kuchangia jumla ya Sh.53,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inaunga mkono nguvu na jitihada za wananchi na wadau wa maendeleo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tumpongeze Mheshimiwa Butondo kwa kufuatilia kwa karibu masuala yanayohusu usalama wa raia na mali zao na uhamasishaji wa wadau kuchangia hizi fedha. Nimwahidi tu kwamba Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi tuna mpango mkakati wa kuimarisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Mikoa na Wilaya ambazo hazina kabisa. Kwa hiyo hali ya fedha itakaporuhusu, Wilaya ya Kishapu ni moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Supplementary Question 3

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ujenzi wa Vituo vya Polisi unakwenda sambamba na ujenzi wa makazi ya askari ili kuwawezesha Askari Polisi kupata makazi mazuri na kuweza kufanya kazi zao vizuri. Je, ni upi mpango wa Wizara kusaidia suala la nyumba za askari polisi katika eneo la Kigoma Mjini ambazo ziko katika hali mbaya sana?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ng’enda,
Mbunge wa Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba askari wanahitaji makazi hususan yawe karibu na vituo vya polisi, lakini tunajua pia kwamba makazi mengi hasa vituo vya zamani ni mabovu, ndio maana kipaumbele kimewekwa kwenye ukarabati wa majengo yaliyochakaa. Hata hivyo, tutaendelea kuimarisha ujenzi wa nyumba kwa ajili ya makazi ya askari kadiri tutakavyoweza kupata fedha kutoka Serikalini.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa wananchi wa Kata ya Saja, Kijombe, Uhenga ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe wako mbali sana na huduma za kipolisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi ndani ya Kata ya Saja ili kuwapa unafuu wananchi hawa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Neema amekuwa mara kwa mara anaulizia masuala ya ulinzi, lakini jambo moja analonivutia ni kwamba kiwango cha uhalifu Njombe hakilingani na maeneo mengine hasa ile ya mipakani. Kwa hiyo niwapongeze wananchi kwa kuzingatia hilo. Kwa hivyo kadri hali ya fedha itakavyoruhusu tutaendelea kuimarisha kujenga vituo vya polisi katika maeneo yanayohitajika ikiwemo hii Kata aliyoitaja ya Saja kule Njombe.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Kituo cha Polisi cha Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kilichopo Selamagasi kimejengwa toka enzi ya mkoloni na kimechakaa sana. Je, ni nini mpango wa Serikali kukarabati kituo kile?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, Shinyanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu ya baadhi ya maswali ya Wabunge, tunatambua uwepo wa uchakavu mkubwa kwa baadhi ya Vituo vya Polisi kikiwemo hiki alichokitaja.

Mheshimiwa Spika, kama tulivyosema alivyosoma hotuba ya bajeti ya Wizara hii mpango wa Serikali kuanza ukarabati wa Vituo vya Polisi na makazi katika mwaka ujao na fedha zimepitishwa, tutaangalia kiwango cha uchakavu ili kuweza kuweka kipaumbele vikiwemo hivi vya Wilaya ya Shinyanga.