Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 200 2022-05-16

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba uliokwama kwenye ngazi ya lenta kwa miaka mitatu sasa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chemba ulianza mwezi Novemba mwaka 2018. Gharama za jumla za ujenzi huu ni Sh.296,000,000. Ujenzi huo umeshirikisha nguvu za wananchi pamoja na Mdau aitwaye Local Investment Climate ambaye alitoa kiasi cha Sh.43,000,000. Ujenzi umefikia kwenye hatua ya lenta na ulisimama kutokana na kukosekana kwa fedha. Kiasi cha Sh.53,000,000 tayari kimeombwa kwenye mfuko wa tuzo na tozo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ili kumalizia ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.