Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa katika Shule ya Msingi Kingurungundwa iliyopo Mchinga?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Lakini kutokana na umuhimu wa shule hii, kama ilivyoelezwa hapa; kwamba ni ya muda mrefu sana; na naona hapa majibu yote yaliyotoka ni ya jumla jumla.

Mheshimiwa Spika, nachotaka kuomba ni commitment ya Serikali; je, Shule hii ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha kufanyiwa ukarabati? Kwa sababu hali ya shule hii ni mbaya zaidi kuliko hizo shule nyingine ambazo umezijumuisha kwenye majibu yao. Naomba kupata commitment ya Serikali, hii Shule ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha ili ifanyiwe ukarabati mkubwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI
ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tulijibu katika jibu la msingi, kwamba, mpango wetu wa sasa ni kuzifanyia tathmini shule zote ikiwemo shule ya Kingurungundwa. Tukishamaliza mchakato; maana yake ni kuanzia mwaka huu wa fedha mpaka mwaka 2025/2026. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba tutafanya mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha shule hiyo inafanyiwa ukarabati, ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa katika Shule ya Msingi Kingurungundwa iliyopo Mchinga?

Supplementary Question 2

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Na mimi napenda kuuliza swali moja la nyongeza; Shule ya Msingi Chunya Mjini pamoaja na Shule ya Msingi Chunya Kati ni shule kongwe ambazo zilikuwepo tangu kabla nchi yetu haijapata uhuru. Shule hizi zimechakaa sana baaddhi ya majengo yameanguka.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha ili ukarabati wa majengo hayo uweze kufanyika na ziweze kurudi katika hali kama shule nyingine ambazo zinajengwa sasa hivi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kitu kikubwa ambacho nikukuhakikishie tu kwamba miongoni mwa shule ambazo ziko katika mpango hizi ni mbili ambazo umezianisha Mheshimiwa Mbunge, na tutahakikisha baada ya tathmini tutazipa kipaumbele ili kuhakikisha kwamba zinajengwa. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa katika Shule ya Msingi Kingurungundwa iliyopo Mchinga?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Shule ya Msingi SUA ambayo ina matatizo ya upungufu wa vyuo itafanyiwa ukarabati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu tathmini yetu itaisha mwezi Julai 2022 na tutakuwa na shule zote nchini, ikwemo ya Shule ya Msingi SUA ambayo ameiainisha hapa. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba mara baada ya hiyo tathmini kila mmoja atajua shule yake inahudumiwa lini. Ahsante sana.