Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 197 2022-05-16

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa katika Shule ya Msingi Kingurungundwa iliyopo Mchinga?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsate sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuna shule za msingi kongwe 2,147 nchini ambazo zilianzishwa kabla ya kupata Uhuru mwaka 1961. Hali ya miundombinu ya shule hizo ni mseto zikiwemo zenye hali nzuri na nyingine zenye miundombinu chakavu.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais-TAMISEMI imeanza kufanya tathimini ya hali ya miundombinu ya shule zote za msingi kupitia mradi wa BOOST ili kubaini mahitaji ya ujenzi wa miundombinu mipya ya shule na hali ya uchakavu wa miundombinu iliyopo. Tathimini hiyo imeanza mwezi Aprili, 2022 na itakamilika mwezi Julai, 2022.

Mheshimiwa Spika, matokeo ya tathimini hiyo yatatumika kuandaa mpango wa uendelezaji na ukarabati wa miundomibinu ya shule za msingi kwa miaka mitano, kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi mwaka 2025/2026 ikiwemo Shule ya Msingi Kingurungundwa.