Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa tatizo la vifo vya akinamama katika Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, je, sasa Serikali imeshafanya utafiti kujua ni watumishi wangapi watawapeleka, na je, kwenye hizi ajira mpya watapeleka watumishi wangapi kwa ujumla? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake specific kwa Mkoa wa Mwanza kwamba tutapeleka watumishi wangapi, labda tu nimwambie kwamba inajulikana kwamba kwenye level ya zahanati wanahitajika watumishi wangapi, kwenye level ya kituo cha afya inahitajika watumishi wa wangapi kwenye level ya hospitali ya wilaya wanahitajika watumishi wangapi mpaka tunapofika Taifa. Lakini kama kawaida kutokana na bajeti na uwezo wa Serikali imekuwa si rahisi kuhakikisha tunawapata wote kwa wakati mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali ilitangaza juzi ajira 32,000 nimuombe Mheshimiwa Mbunge ili nisije nikamwambia data ambazo si sahihi tuje tukae tuangalie specifically Mkoa wa Mwanza kwenye ajira hizi wanapata watumishi wangapi kwenye eneo hilo.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa tatizo la vifo vya akinamama katika Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 2

STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kujua. Pamoja na maandalizi ya vifaa kwenye vituo vinavyojengwa, tunavyo takribani vituo vinne ambavyo vimeshakamilika; kule Igoma, Fumagila, Bulale pamoja na Nyegezi;

Ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kupeleka vifaa kwenye vitu hivi ambavyo vipo tayari na kuanza kutoa huduma? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele sasa cha Wizara ya Afya na Waziri wa Afya ameshaelekeza wataalam wote, kwamba vituo vingi sasa vimeshakamilika na ujenzi wa kwa kiasi kikubwa sasa umeshafanyika.

Sasa kipaumbele cha kwanza ni kuhakikisha kuwa vituo ambavyo vipo tayari vinaanza kazi na kuhakikisha vina vifaa na watumishi. Kwa hiyo ndani ya mwaka huu kabla ya mwezi wa 10 vituo vyote vitakuwa vimepata vifaa tiba na vitakuwa vimeanza na wataalam watakuwa site. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa tatizo la vifo vya akinamama katika Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kutupa mrejesho wa vifo vya uzazi vinavyotokana na uzembe ili tuweze kuwa na imani kwamba Serikali inafuatilia? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kila kifo kinachotokea cha mama anayejifungua huwa kinajadiliwa. Sasa, anasema kwamba ni lini wataanza kutupa mrejesho; kwakweli ni kazi yetu pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwetu Mheshimiwa Waziri wa Afya ameshaelekeza, na kwamba tumegundua watu kama Red Cross wana mtandao mkubwa sana kutoka taifa mpaka tunafika kwenye vitongoji vyetu na ni mtandao wa kijamii. Tunafikiri kwamba tukiwashirikisha hao, tunataka sasa, kama ilivyo elimu, kwenye vituo vyetu vya afya na zahanati zetu kuwepo na ownership wa kijamii, kwamba kila tatizo linapotokea liwepo wanajamii wanajadili inajulikana kwenye jamii na information zinaenda vizuri kwenye jamii. Kwa namna hiyo tutaweza kupunguza vifo vya akina mama

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile sisi wanaume tunahitaji kuwa na ownership ya ujauzito wa akina mama tangu mama anavyobeba mimba tuweze kushirikiana na mama mpaka siku anapojifungua. Tukifanya hivyo nayo itatusaidia vizuri sana kwasababu kila baba anapenda kujisifia mtoto wake ambaye anafaulu vizuri shuleni, lakini kufaulu kwa mtoto vizuri shuleni kunaendana vilevile na kuanza kutunza mimba toka siku mimba inavyobebwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo akinababa kama tunapenda watoto wafanya vizuri shuleni wawe brilliant kwenye maisha tuanze na mimba siku mama anapobeba ujauzito. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna hiyo suala la afya litakuwa sio suala la wataalam wa Afya peke yao, litakuwa suala la kijamii. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa tatizo la vifo vya akinamama katika Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 4

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Takwimu zinaonesha Watanzania takribani milioni kumi na tano, sawasawa na asilimia 34.2 ni maskini kabisa.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuleta Muswada wa Bima ya Afya kwa kadri ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais ili akina mama wajawazito waweze kupata huduma ya afya na kupunguza vifo vyao?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jibu swali zuri la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba, kama mnavyojua Wabunge, tayari kwenye Kamati ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii tumewaelezea na tumewafafanulia hatua tulizozifikia kwenye suala zima la bima ya afya. Na nafikiri Bunge zima limeshaelekeza sisi Wabunge tuna uchaguzi. Kwa sababu ukiangalia mtu anaweza akasubiri akaacha kuweka luku kwenye nyumba yake umeme usiwepo na akasubiri kesho lakini akiugua haiwezi kusubiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anaweza akaamka akiwa na afya yake kufuata maji mbali zaidi, lakini afya hawezi hata iliyopo ndani ya nyumba yake hawezi.

Kwa hiyo ni uchaguzi wetu, tutakapoleta Mswada tuamue tunapata vyanzo gani ambavyo vitatusaidia kuweza kuweka kwenye mfuko wa afya; tupate bilioni 149.77 ambazo zitatusaidia na kuwasaidia wale Watanzania wasioweza kujilipia mfuko wa mima ili sasa tufikie hatua ya sisi kuanzisha bima ya afya kwa wote. Ahsante sana Wabunge. (Makofi)