Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 196 2022-05-13

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa tatizo la vifo vya akinamama katika Mkoa wa Mwanza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali ya Mheshimiwa kabula Enock Shitobelo Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeimarisha huduma za akina mama kujifungulia katika vituo vya huduma katika Mkoa wa Mwanza kwa kujenga vituo vya afya 22 vinavyotoa huduma za upasuaji, na inaendelea na ujenzi wa vituo vya afya 15 vitakavyotoa huduma za upasuaji mara vitakapokamilika. Aidha, serikali imeimarisha utoaji wa elimu ya Afya ya uzazi kuhusu viashiria vya hatari kwa akina mama wajawazito na kupitia ajira mpya zilizotangazwa itapeleka wataalamu zaidi ili kuhakikisha akina mama wajawazito wanapata huduma sahihi kutoka kwa wataalamu, ahsante. (Makofi)