Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanza Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru Serikali kwa majibu mazuri juu ya kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Mto Ruichi. Nina swali moja la nyongeza. Jimbo la Buhigwe lina skimu mbili, skimu ya Rukoyoyo na skimu ya Mugera ambazo nazo hazijawahi kupata msaada wowote kutoka Serikalini.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuziendeleza skimu hizi za Rukoyoyo na Mugera zilizoko katika Wilaya ya Buhigwe?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango mkakati, tulioweka Wizara ya Kilimo ni kuhakikisha skimu zote za umwagiliaji hapa nchini zinafanya kazi. Hivyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, ya kwamba katika bajeti yetu inayokuja itakayosomwa wiki ijayo wataona miradi mingi ambayo tumeainisha kwa ajili ya kuifufua, kuikarabati na kujenga upya ambapo pia naamini itagusa katika mikoa mingi ikiwemo Mkoa wa Kigoma. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanza Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Serikali iliahidi kukamilisha miradi ya umwagiliaji ya skimu ya Karema na skimu ya Kabaki. Kupitia kwa Waziri aliyekuwpepo aliahidi kuwa atakamilisha hiyo miradi.

Je ni lini itakuja kukamilisha hiyo miradi miwili ndani ya Wilaya ya Tanganyika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi Seleman Kakoso Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, skimu alizozitaja Mheshimiwa Mbunge, mimi nimefika na nilitoa pia ahadi hii mbele ya wananchi wake katika mkutano wa adhara ambao tuliufanya pale kijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti inayokuja ya mwaka 2022/23 miradi wa skimu hizi imeainishwa na itatekelezwa kupitia bajeti hiyo inayokuja. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tuliipokea na tunaendelea na utekelezaji wa miradi hiyo.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanza Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Serikali iliwekeza zaidi ya milioni 700 kwenye Bonde la Miogwezi lililoko kwenye Kijiji cha Igongo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji, lakini mradi ule umesimama.

Je, Mheshimiwa Waziri huu nao ni kati ya miradi itakayotekelezwa kwenye mwaka wa fedha 2022/ 2023?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi linaloendelea hivi sasa ambapo ni maelekezo wamepewa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika kuhakikisha kwamba miradi yote hii inafanya kazi. Tumewapa jukumu la kupitia miradi yote nchi nzima kujua status yake, tuone ipi inafanya kazi, ipi inahitaji marekebisho na ipi inahitaji over whole, kwa maana ya kuanza upya katika mradi husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kwamba katika bajeti yetu ambayo tutaisoma wiki inayokuja tutaainisha miradi ambayo itatekelezwa na imani ni kwamba katika mradi aliosema tutaingiza katika utaratibu wa utekelezaji katika bajeti inayokuja.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanza Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 4

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Katika Kata ya Msia pana bwawa dogo ambalo lipo katika Kijiji cha Msia. Bwawa hili linaweza kutumika sana katika kilimo cha umwagiliaji hasa katika mashamba ya kahawa. Na kwa muda mrefu limekuwepo kwenye bajeti lakini Serikali haijaweza kutekeleza. Ni lini Serikali itaanza kutekeleza lile bwawa ili liweze kutumika katika kilimo cha umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hasunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha ya kwamba ifikapo mwaka 2025 tumekuwa na eneo la umwagiliaji la hekta milioni moja na laki mbili yakiwa ni maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, ya kwamba katika kufikia azma hiyo ni lazima pia tutekeleze miradi mingi kadri iwezekanavyo ili wananchi wengi waweze kunufaika. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba bwawa alilolisema tutaelekeza wataalamu katika bwawa la pili pia kulipitia ili waje watushauri vizuri namna ya utekelezaji wake lakini ni jambo ambalo ndani ya wizara tunaona kwamba ni jambo muhimu na hivi sasa changamoto kubwa ni upatikanaji wa mabwawa yenye uhakika wa maji. Kama bwawa lipo tayari ni njia rahisi zaidi ya kuanza utekelezaji wa mradi. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge tutalisimamia hilo na mradi utatekelezeka.