Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 191 2022-05-13

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanza Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche Mkoani Kigoma?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche lililopo katika manispaa ya Kigoma Ujiji mkoa wa Kigoma. Bonde hilo linauwezo wa kumwagilia hekta 3,000 na kunufaisha wakulima wa vijiji vitatu vya Mahembe, Nyangofa na Kidawe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa skimu hii utaanza mwaka wa fedha 2022/2023. Utekelezaji wa mradi huu unafadhiliwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (Kuwait Fund for Arab Economic Development) ambapo litajegwa bwawa lenye mita za ujazo milioni 70, ujenzi wa mfereji mkuu Kilomita 10 na mifumo ya umwagiliaji. Serikali imepata kibali (No Objection) kutoka kwa wafadhili mwezi Aprili, 2022 kwa ajili ya kufanya mapitio ya usanifu na kutafuta mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Luiche.