Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI E. KINGU K.n.y MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuwaingiza Wazee na Wanaume kwenye mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri kwa kuwa kwa sasa wameachwa?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI E. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa fedha hizi asilimia kumi zinazotolewa kama mikopo zinatokana na tozo pamoja na kodi ambazo wananchi kwa ujumla wengi wanashiriki kuzitoa na zinazokusanywa katika halmashauri yetu;

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuwapitia vijana wote mikopo bila kuwabagua, kama vile Serikali vijana wengi waliojiajiri katika sekta za uzalishaji, ujasiriamali, kilimo na boda boda,?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wanaume, kwa maana ya akina baba nao pia wamekuwa wakijishughulisha na shughuli za uzalishaji. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuwapatia nao mikopo bila kuwabagua?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Elibariki Kingu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba asilimia kumi inatokana na mapato ya ndani na inagusa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Na niseme dhahiri kwamba mikopo hii haina ubaguzi wowote kwa vijana, kwa wanawake, wala watu wenye ulemavu. Suala ambalo wanatakiwa kufanya kwa mujibu wa sheria na kanuni za asilimia kumi ni kuomba kupitia vikundi vyao vya ujasiriamali. Na vijana wote wanaomba kupitia vikundi na wakawa na sifa hizo hakuna anayebaguliwa, wote wanapewa mikopo hiyo katika mazingira ya halmashauri zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutaendelea kuhakikisha kwamba tunawapa fursa vijana wote wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kujiendeleza katika shughuli za kiujasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la wanaume, utoaji wa mikopo hii ni kwa mujibu wa sheria, na sheria yetu ambayo tuliipitisha katika Bunge hili ilisema vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu. Vijana ni umri wa chini wa miaka 35, lakini hoja ya msingi ni kwamba wanaume walio wengi ukilinganisha na makundi haya tayari wanauwezo wa kuwa dhamana, kwa maana ya ardhi, majengo na biashara ambazo zinaweza kutumika kama collateral kwenye mikopo ukilinganisha na makundi haya. Ndiyo maana tuliweka kipaumbele kwa wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu kwa sababu hawana collaterals zinazowawezesha kupata mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kufanya tathmini kuona uwezekano wa kuingiza wanaume kwa kadri itakavyoona inafaa. Ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI E. KINGU K.n.y MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuwaingiza Wazee na Wanaume kwenye mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri kwa kuwa kwa sasa wameachwa?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa walemavu hawa si wote wana uwezo wa kufanya shughuli za kibiashara ama kujiwezesha kiuchumi lakini wanalelewa na babu zao, bibi zao ama baba zao ama wajomba zao ambao hawa-qualify katika hii asilimia kumi.

Je, Serikali haioni wakati umefika sasa wakuangalia wazazi ama walezi wanaoangalia walemavu ambao wenyewe hawajiwezi lakini wanaweza kuwezeshwa kwa ajili ya kuangalia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna walemavu ambao hawana uwezo wa kufanya shughuli hizo na wangehitaji kupata mikopo ili wajikwamue kiuchumi. Naomba tuchukue wazo la Mheshimiwa Mbunge, tukalifanyie tathmini na kuona uwezekano wa kuwapa mikopo hiyo wazazi au walezi wa hao wenye ulemavu ili waweze kuwasaidia. Ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIBARIKI E. KINGU K.n.y MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuwaingiza Wazee na Wanaume kwenye mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri kwa kuwa kwa sasa wameachwa?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kutokana na majibu ya msingi ya swali hilo, Mheshimiwa Waziri ameendelea kusisisitiza kwamba mikopo hiyo inatolewa kwa vikundi; na kwa kuwa hiyo dhana ya vikundi imekuwa ni mwiba sana kwa wale akina mama wa Kilimanjaro wanaotaka kuchukua mikopo hususan wale ambao wako katika ujasiriamali.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kurekebisha kipengele hicho ili mikopo hiyo itolewe kwa mtu mmoja mmoja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kuipitia sheria na kanuni ya mikopo ya asilimia kumi. Katika kupitia kanuni hii tayari tumeshaanza kufanya tathmini kwa kina ili kuona maeneo gani yanahitaji kuboreshwa zaidi likiwemo suala la kuona uwezekano wa mtu mmoja kupata mkopo badala ya vikundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, baada ya tathmini hiyo, tutafanya maamuzi na kuona utaratibu sasa utakuwa wa aina gani. Ahsante.