Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 190 2022-05-13

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ELIBARIKI E. KINGU K.n.y MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: -

Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuwaingiza Wazee na Wanaume kwenye mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri kwa kuwa kwa sasa wameachwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa Mbunge wa Jimbo la Ukonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa sheria ya mikopo ya asilimia 10 na kanuni zake, mikopo hii inatolewa kwa ajili ya kuwezesha makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupata mikopo yenye masharti nafuu. Makundi haya kwa kiasi kukubwa hayawezi kupata mikopo katika taasisi nyingine za fedha kwa sababu ya kukosa dhamana na uwezo mdogo wa kumudu riba ili waweze kushiriki katika shughuli za kiuchumi na kujiongezea kipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kufanya tathmini ya utoaji na urejeshaji wa mikopo hii tangu kutungwa kwa sheria. Tathimini hii itawezesha kushauri namna bora ya utoaji wa mikopo pamoja na mapitio ya Sheria. Ahsante.