Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je ni lini Kituo cha Afya Mapera kilichopo Mbinga Vijijini Kitaanza kutoa huduma za Mionzi na Ultra sound?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana na nishukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kituo hiki cha Mapela, ndio kituo pekee cha Serikali katika Halmashauri ya Mbinga Vijiji ambayo ina kata 29. Hicho kituo cha Maguo alichokitaja Mheshimiwa Naibu Waziri ni kituo cha Mission, tu nashukuru wanatusaidia, sina hakika kama gharama zake zinalingana, sina hakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti nina maswali maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni lini Serikali itapeleka wahuduma wa afya, katika zahanati saba Kipolopolo, Lukiti, Kihuruku, matuta, Mwihayo, Ikwela na Lituru; zahanati hizi nimeuliza mwaka jana swali hapa. Lini zitafunguliwa maana wananchi wamejenga na wamekamilisha, lini sasa zitafunguliwa ili ziweze kutoa huduma kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Halmasauri ya Mbinga, ina upungufu mkubwa wa watumishi, zaidi ya asilimia 80 hatuna watumishi. Je, katika mgao huu unaokuja, Serikali ipo tayari kuwaonea huruma na kutoa kipaombele katika halmashauri ya Wilaya ya Mbinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Halmashauri ya Mbinga Vijijini ina kata 29 na ina kituo kimoja cha afya; lakini nimuhakikishie Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Hassan ameweka mkakati wa uhakika wa kujenga vituo vya afya vya kimkakati katika kata za mkakati na tarafa za kimkakati. Tulishakuomba na ulishaleta hapa orodha ya kata ambazo zitajengewa vituo vya afya. Nikuhakikishie Serikali hii sikivu tutahakikisha tunajenga vituo vya afya katika Jimbo la Mbinga Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, kuhusiana na watumishi kuhitajika katika zahanai saba; kwanza niwapongeze sana wananchi wa Mbinga Vijijini kwa kutoa nguvu kujenga zahati saba ambazo zimekamilika, lakini na Serikali ilichangia. Nimhakikishie kwamba tunakwenda kuzisajili zahanati hizi. Kwa upande wa ajira hizi ambazo zimetangazwa tutakwenda kutoa kipaumbele kikubwa kwenye halmashauri zote zenye upungufu mkubwa wa watumishi ikiwepo Halmashauri ya Mbinga Vijijini. Ahsante.