Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 189 2022-05-13

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je ni lini Kituo cha Afya Mapera kilichopo Mbinga Vijijini Kitaanza kutoa huduma za Mionzi na Ultra sound?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI , OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya cha Mapera kilipokea fedha Shilingi Milioni 400 mwaka wa fedha 2019/ 2020 kwa ajili ya ukarabati mkubwa na upanuzi wa Kituo. Kituo hicho kimekamilika na kuanza kutoa huduma za upasuaji toka Julai 2021 na jumla ya Wakinamama 114 wamekwisha pata huduma ya upasuaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wananchi wa Kata ya Mapera wanapata huduma ya X- Ray kwenye Kituo cha Afya cha Maguu kilichopo kilometa tatu kutoka kwenye Kituo cha Afya Mapera. Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga inashauriwa kutenga fedha kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kujenga jengo la X-ray ili Serikali ikipatie Kituo hicho mashine ya X-ray. Ahsante.