Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni vigezo gani vinapaswa vifuatwe na halmashauri ili fedha za maendeleo ziweze kutolewa?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kwanini sasa Serikali haina mikakati ya kuhakikisha kwamba halmashauri zenye vyanzo vidogo vya mapato iweze kuwa inawapa fedha nyingi kuliko ambazo zinatengwa ukilinganisha na halmashauri nyingine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kwanini Serikali isitumie vigezo vya ukubwa wa eneo ili kuhakikisha kwamba inatoa fedha kulingana na kipaumbele, kulingana na ukubwa wa eneo husika, kuliko wanavyofanya sasa hivi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE.DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vyanzo ambavyo halmashauri wanakusanya kwa mapato ya ndani vinatofautiana kati ya halmashauri moja na nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hoja ya Mheshimiwa Mbunge, kwamba zile halmashauri zinazopata mapato kidogo ya ndani zipewe fedha zaidi. Ni kwamba suala hili linakwenda kuzingatia pia mara nyingi, ukiziona halmashauri hizi zenye mapato madogo ni halmashauri pia ambazo zina population ndogo lakini pia zina shughuli za kibiashara ndogo zaidi ukilinganisha na halmashauri zenye mapato makubwa kwa sababu mapato yanatokana na shughuli za kiuchumi katika halmashauri husika.

Kwa hiyo, utaratibu wa kupeleka fedha unazingatia pia population ya eneo husika, lakini pia na shughuli zile, kwa mfano miradi ya kimkakati ambayo ilitakiwa kwenye kuwekezwa kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tutaendelea kufanya tathmini kuona uwezekano wa kuongeza zaidi package za maendeleo kwa halmashauri zenye mapato madogo, ukilinganisha na halmashauri zenye mapato makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na kuzingatia ukubwa wa eneo la kijiografia, suala hili linategemeana na ukubwa lakini pia population kwa sababu fedha za maendeleo zinapelekwa kwa ajili ya kusaidia wananchi. Kuna halmashauri ambazo ni kubwa sana zina maeneo ya hifadhi za misitu na kadhali. Kwa hiyo, ukiangalia tu ukubwa wa jiografia utapeleka fedha nyingi eneo ambalo lina population ndogo kwa sababu tu kuna ukubwa wa jiografia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunazingatia yote, ukubwa, population lakini pia na shughuli zingine za kimaendeleo.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni vigezo gani vinapaswa vifuatwe na halmashauri ili fedha za maendeleo ziweze kutolewa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali imekuwa ikitoa fedha za maendeleo kwenye halmashauri wakati mwingine imekuwa ikitoa fedha mwezi ambao unakaribia mwisho wa mwaka wa fedha kuisha.

Je, Serikali imetatua vipi changamoto hii ya kuchelewesha fedha kwenye halmashauri na baadaye kuzirudisha hazina?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE.DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ambazo zinapelekwa kwenye halmashauri zetu karibu na mwisho wa mwaka wa fedha mara nyingi zimekuwa zikirejeshwa kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti Na. 11 ya Mwaka 2015.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo mahususi yametolewa, kuhakikisha kwamba halmashauri ambazo zinapokea fedha karibu na mwisho wa mwaka wa fedha, ziandike barua kupitia ofisi ya Rais TAMISEMI, kwenda Wizara ya Fedha na Mipango, siku 15 kabla ya tarehe 30 ya mwaka husika, ili zile fedha zisirejeshwe ziendelee na miradi, kwa maana ya quarter ya kwanza ya mwaka wa fedha unaofuata.