Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 188 2022-05-13

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, ni vigezo gani vinapaswa vifuatwe na halmashauri ili fedha za maendeleo ziweze kutolewa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utoaji wa fedha za maendeleo zilizotengwa katika bajeti hutolewa kwa halmashauri kwa kuzingatia Waraka na Mwongozo wa Wizara ya Fedha na Mipango kila mwaka kwa kuzingatia maelekezo ya Kifungu Na. 5 cha Kanuni za Sheria ya Bajeti Sura 439, Kifungu cha 6 cha Sheria ya Fedha za Umma, Sura 348 na Kifungu cha 12 cha Sheria ya Bajeti Sura 439.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya vigezo hivyo ni pamoja na halmashauri kuwasilisha maombi ya fedha za utekelezaji ikionesha utayari wa kuanza kutekeleza mradi mara baada ya kupokea fedha. Ahsante.