Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nimeridhika na majibu hayo ya Serikali, lakini nimepata wasiwasi juu ya ufuatiliaji wa kazi hii. Barua ya hati miliki tu imechukua miaka miwili tangu Aprili, 2020 mpaka leo 2022 hakuna majibu yoyote. Je, Mheshimiwa Waziri ananiahidi nini kunitoa wasiwasi huu juu ya ufuatiliaji wa kazi hii?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Hija, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana naye kwamba si kawaida kuchukua muda mrefu namna hii hasa baada ya Jeshi la Polisi kuwa wamelipa Sh.2,200,000 kwa ajili ya kupata hati ya kiwanja hicho. Tutafuatilia kwa karibu na kupitia hadhara hii, nimwombe Kamishna wa Polisi Zanzibar afanye ufuatiliaji yeye binafsi ili kuhakikisha kwamba hati inapatikana, hatimaye ujenzi kwenye eneo hili uweze kuanza. Nashukuru.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM A. MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kijiji cha Vujini, Wilaya ya Mkoani kina matokeo ya uhalifu sana. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika kijiji hicho ili kupunguza matukio hayo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa hali ya usalama Zanzibar. Niombe tuendelee kushirikiana ni kweli kwamba baadhi ya maeneo ya Zanzibar ikiwemo kijiji alichokitaja kina hayo matukio ya uhalifu, lakini Jeshi la Polisi linafanya misako na doria kule ambako hakujawa na kituo ili kuhakikisha kwamba usalama unakuwepo. Kwa hiyo tutawasiliana na wenzetu wa upande wa Zanzibar kama maeneo yamepatikana na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano, basi kituo hicho kinaweza kuanza kujengwa kwa siku za usoni.

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Supplementary Question 3

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wilaya ya Ilemela inajenga Kituo cha Polisi kwa nguvu za wananchi eneo la Nyamuhongolo. Aliyekuwa Waziri wa Mambo na Ndani Mheshimiwa Kange Lugola alitoa ahadi ya mifuko 100 ya cement. Je, ni lini Wizara ya Mambo ya Ndani itatimiza ahadi hiyo? (Makofi/Kicheko)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Mwanza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze wananchi wa Ilemela pamoja na halmashauri yao kwa kuanza ujenzi wa kituo cha Polisi eneo la Nyamuhongolo tunawaunga mkono. Tutafuatilia ikiwa kweli Waziri wetu alitoa ahadi hiyo kuona uwezekano wa kuitekeleza ili isionekane kwamba Serikali inadanganya raia wake. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Maswa ni wilaya kongwe, lakini mpaka sasa haina Kituo cha Polisi.

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi Wilaya ya Maswa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunatambua kwamba Maswa ni wilaya kongwe katika Mkoa wa Simiyu lakini inacho kituo cha polisi ambacho ni chakavu na kwa kweli ni majengo ya kuazima. Tutawasiliana na uongozi wa mkoa ili kupata eneo, hatimaye kuweka mipango ya ujenzi wa vituo vya polisi kwenye maeneo ambayo hayana ikiwemo Wilaya ya Maswa. Nashukuru.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Supplementary Question 5

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kutokana na kadhia ambayo ipo katika swali la msingi ambalo lililoulizwa, Jimboni kwangu katika Jimbo la Chumbuni nimekuwa nikiahidiwa ahadi kama hizi zaidi ya mwaka wa nne huu sasa hivi na Bunge lililopita Naibu Waziri alisema akija Zanzibar atakuja kwangu, lakini hakuweza kufika. Je, leo hii ananiahidi nini ili tukimaliza Bunge hili aweze kushughulikia vituo vyangu vya Chumbuni? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Nyongeza la Mheshimiwa Pondeza, kama ifuatavyo na kwa kweli kama nimemsikia vizuri: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli niliahidi kwenda Zanzibar na moja ya maeneo ambayo ningetembelea ni eneo alilolibainisha, lakini kutokana na ratiba kuwa finyu, nilishindwa kufika. Ipo ahadi ambayo niliitoa kuhusu kumalizia Kisiwa cha Pemba. Nitakapokwenda kule, eneo lako pia nitalitembelea ili kuona changamoto iliyopo. Nashukuru. (Makofi)