Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 180 2022-05-11

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tumbatu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga kituo cha Polisi na nyumba za makazi ya askari katika eneo Tumbatu wilaya ya Kaskazini “A” kwani eneo hilo ni kisiwa. Jeshi la Polisi liliomba na kupewa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba elfu 47.5 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi pamoja na nyumba za makazi ya askari. Jeshi la Polisi kupitia Kamisheni ya Zanzibar iliwasilisha maombi ya kupewa Hati miliki ya eneo hilo kwenye Mamlaka husika yaani Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “A” kupitia barua yenye Kumb.Na.PHQ/Z/C-5/17/X/41 ya tarehe 4 Aprili, 2020. Kinachosubiriwa ni kupata hati ya umiliki ili kuanza taratibu za kuomba fedha kwenye bajeti ya Serikali kwa ajili ya ujenzi nashukuru.