Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya kutia moyo ya Serikali, shule za msingi 459 za Wilaya za Misenyi, Ngara, Biharamulo, Bukoba Vijijini pamoja na Muleba katika Mkoa wa Kagera hazijaunganishwa na maji safi na salama. Kwa hiyo ningependa kupata commitment ya Serikali ni nini itakwenda kufanya kuhakikisha shule hizi zinaunganishwa na maji safi na salama ili kutoendelea kuweka hatari afya za watoto zaidi ya laki nne wanaosoma kwenye shule hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mtaa wa Kisindi na Kashenye katika Kata ya Kashai, Bukoba Manispaa ina changamoto kubwa sana ya maji. Je, Wizara hii itakwenda kufanya nini kupata ufumbuzi wa haraka ili kutua ndoo akinamama ambayo ndiyo dhamira ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nampongeza sana Mheshimiwa Neema kwa ufuatiliaji mzuri. Suala la maji mashuleni, kwenye vituo vya afya, kama nilivyoongea kwenye maswali mengine, hili ni agizo ambalo Wizara imetoa kwa watendaji wote mikoani. Hivyo nitarajie mabadiliko makubwa sana katika shule zote za Mkoa wa Kagera zitafikiwa na maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la maji katika mitaa aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge dhamira ya Mheshimiwa Rais ni kuona kwamba watu wote wanafikiwa na maji safi na salama na ya kutosha, hivyo mitaa hii pia naamini kabla ya mwaka huu wa fedha haujaisha, wataweza kupatiwa huduma ya maji safi na salama na ikiwezekana basi kufikia mwaka ujao wa fedha pia zoezi litaendelea ili kuona maeneo yote yanapata maji safi na salama.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niseme tu ukweli kwamba, Mheshimiwa Naibu Waziri ni miongoni mwa viongozi wakweli sana. Sasa naomba Mheshimiwa Naibu Waziri au Serikali ituambie, kwenye ule Mradi wa Miji 28 bomba kutoka Tabora kwenda Sikonge litaanza kulazwa lini? Nashukuru sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nikushukuru kwa pongezi. Kwenye hii mijii 28 hivi karibuni tunamtarajia Mheshimiwa Rais aweze kushiriki katika kusaini ambapo sasa kazi zitaanza na bomba hilo litalazwa mara baada ya mradi huu kuanza kufanyiwa kazi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini liko ukanda wa juu wa Rift Valley visima vingi vilivyochimbwa na Serikali kwenye Shule na Taasisi nyingi vimekauka. Bahati nzuri tuna Ziwa Basutu tuna ziwa Madunga, je, ni nini mpango wa Serikali wa kupeleka maji kwenye Jimbo hilo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mbulu Vijijini tayari huduma ya maji inaendelea kupatikana kwa wananchi. Maeneo ambayo maji bado hayajafika tunaendelea na kazi. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kuvuta subira, maeneo yake yote ya Jimbo yatafikiwa na huduma ya maji safi na salama.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji katika Mji wa Kisesa, Bujora, Bukandwe na Bujashe katika Wilaya ya Magu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Matondo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote na yeye nimpongeze kwa sababu ni mfuatiliaji mzuri katika masuala ya huduma ya maji. Maeneo ya Kisesa, Bujora na kote alikokutaja Mheshimiwa Mbunge tunatarajia kuendelea kupeleka huduma ya maji safi na salama.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 5

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wakati Taasisi zisizo za Kiserikali zinahamasisha hedhi salama na kwamba kutakuwa na maadhimisho ya hedhi salama tarehe 28 ya mwezi huu, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba katika shule za msingi na sekondari na hasa tunaposema hedhi salama moja ya kikwazo ni ukosefu wa maji. Kwa nini Serikali isiweke kwenye mikakati yake kila mradi wa maji unapoenda mahali popote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ihakikishe maji hayo yanafika kwanza kwenye shule zetu za msingi na sekondari ili kuhakikisha changamoto hiyo ya hedhi salama inaondoka?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hokororo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji tayari tunahakikisha shule, vituo vya afya na zahanati zote zinapatiwa huduma ya maji safi na salama. Kwa kuzingatia hili la watoto wa kike tunapomtua mama ndoo kichwani tunahakikisha pia huyu mama ajaye pia anabaki na afya yake kwa kupata maji safi na salama. Hivyo watendaji wetu mikoa yote wanafahamu hili na wataendelea kulifanyia kazi.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 6

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Utekelezaji wa ujenzi wa vyoo shuleni kupitia program ya usafi wa mazingira inazingatia uwepo wa maji. Je, ni upi mkazo wa Serikali katika uvunaji wa maji katika majengo ya Serikali zikiwemo shule zetu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara itaendelea kuhakikisha shule zote zinapata maji safi na salama pamoja na vituo vya afya. Lengo ni kutimiza kauli ya maji ni uhai na maji yatazingatiwa kufika na Waheshimiwa Wabunge niwatoe hofu, shule zote katika majimbo yetu zitafikiwa na huduma ya maji safi na salama.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 7

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Shule za Jimbo la Kalenga pamoja na Shule ya Kalenga Primary School karibu kabisa na fuvu la Mkwawa haina maji. Je, ni mpango gani wa Serikali wa kuchimba visima sasa badala ya kupeleka maji ya mserereko maana kuchimba visima ni kazi rahisi katika shule zote za Jimbo la Kalenga? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uchimbaji wa visima katika maeneo ambayo ni rafiki tutaendelea kwa sababu tayari tunafanya zoezi hilo. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge wa Kalenga kama eneo lake linafaa kwa visima mantahofu visima vitakuja kuchimbwa na watoto watapata maji shuleni.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba ataingiza mchakato wa kuingiza LUKU za maji ili kudhibiti gharama zisizo sahihi zinazosomwa na wale wanaosoma. Je, huu mchakato umefikia wapi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kimei, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, LUKU za maji tayari katika baadhi ya mikoa imeshaanza kutumika mita hizo ambazo zinatoa uwezekano wa kulipa kulingana na matumizi yako. Mchakato unaendelea kwa mikoa mingine, lakini tayari tuna pilot Mikoa kama Iringa, Mbeya inafanya vizuri kwa baadhi ya maeneo ambayo tayari imefungwa, hivyo tutasambaza maeneo yote ambayo zitaweza kufikia.