Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Water and Irrigation Wizara ya Maji 178 2022-05-11

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha shule zote nchini zinapata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza inapatikana kwenye shule na vituo vya afya kote nchini. Katika kutimiza azma hiyo, Wizara inaendelea na zoezi la kubainisha shule na vituo vya afya vyenye changamoto ya huduma ya maji, kazi itakayokamilika mwezi Juni, 2022. Baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, kuanzia mwaka 2022/ 2023, Serikali itatekeleza mpango maalum wa miaka mitatu wa kupeleka huduma ya maji kwenye taasisi hizo.