Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika Wilaya za Mkoa wa Mara?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali madogo ya nyongeza.

Je, Serikali inawahakikishiaje wananchi wa Tarime, Rorya, Sirari, Nyamwaga, Nyamongo na Serengeti kwamba, mradi huu wa kutoka Ziwa Victoria utaenda kuanza mwaka huu wa fedha 2022/2023?

Swali la pili, wananchi wa Mji wa Tarime kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia chanzo cha maji kutoka Mto Nyanduruma, lakini maji yale ni machafu na yana rangi ya tope.

Je, Serikali ni lini itaweka chujio la maji ili kuwawezesha wananchi wale kupata maji safi na salama? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ghati Chomete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Ghati Chomete kwa maswali mazuri na amekuwa akifuatilia sana hii miradi, kwa sababu ya mashirikiano katika suala la lini maji ya Ziwa Victoria yatatumika, tayari tumeshafikia hatua zote ziko sawa na sasa tunasubiri tu idhini ya kupata nafasi ya Mheshimiwa Rais ili aweze kushiriki katika kusaini ili mradi wa Miji 28 uanze kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la chujio pia tayari ni moja ya mikakati ya Wizara na tunatarajia kufikia mwaka ujao wa fedha nalo pia litapewa kipaumbele.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika Wilaya za Mkoa wa Mara?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Katika Mkoa wa Simiyu tuna Wilaya Tano, lakini Wilaya ya Meatu inaongoza kwa ukame wa maji.

Je, ni lini sasa tutapata maji ya kutoka Ziwa Victoria maana juzi tu Naibu Waziri amefika pale tumepata maji lakini maji yenyewe yameshakuwa ni ya mgao mtatusaidiaje katika Wilaya ya Meatu?(Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Meatu ni kama alivyoeleza Mheshimiwa Mbunge, niliweza kufika mimi mwenyewe na ninakushukuru sana Mheshimiwa Minza kwa ushirikiano wako kwa namna ambavyo tumeweza kupunguza ile changamoto ya maji machafu na sasa hivi angalau mnapata maji kwa zamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ya uhakika kutoka Ziwa Victoria tayari unaendelea kufanyiwa kazi, kama unavyofahamu tayari watu wameshaanza kulipwa fidia zao na ule ni mradi maalum kwa ajili ya mabadiliko ya tabianchi, hivyo tutarajie mwaka huu ujao wa fedha shughuli zote zitakwenda kufanyika vizuri.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika Wilaya za Mkoa wa Mara?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba nimuulize swali la nyongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, Shule ya Sekondari ya Kijombe ina shida sana ya maji ambayo iko ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe. Je, lini Serikali itahakikisha kwamba inapeleka maji katika shule ile kwa sababu ni shule ya bweni ili watoto wetu waweze kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Mbunge Neema kwa ufuatiliaji wa usalama wa watoto wetu na hili ni agizo ambalo tayari Wizara imelitoa katika mikoa yote. Naomba nitumie Bunge lako Tukufu niendelee kuwaagiza watendaji wetu wa Mkoa wa Njombe wahakikishe Sekondari ya Kijombe inapata maji safi na salama.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika Wilaya za Mkoa wa Mara?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Mkoa wa Kigoma umejaaliwa neema ya kuwa na Ziwa Tanganyika na Mto Malagarasi, lakini ni mkoa ambao bado unakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji. Je, nini mkakati wa Serikali kutumia maji ya Mto Malagarasi na Ziwa Tanganyika ili kumaliza uhaba wa maji katika Mkoa wa Kigoma hususan Jimbo la Muhambwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florence, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi ya vyanzo vya maji vya Maziwa Makuu na mito mikubwa ni moja ya mikakati ya Wizara, hivyo Mto Malagarasi na Ziwa Tanganyika navyo pia viko kwenye mikakati ya Wizara kadiri tutakavyokuwa tunapata fedha za kutosha tutatoa kipaumbele kwenye vyanzo hivi vikubwa ili tuendelee kupata miradi endelevu.