Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Water and Irrigation Wizara ya Maji 177 2022-05-11

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika Wilaya za Mkoa wa Mara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Mara kwa sasa ni wastani wa asilimia 66 vijijini na asilimia 71 mijini. Katika kuboresha huduma ya maji katika Mkoa wa Mara, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mikubwa miwili ya Mugango, Kyabakari hadi Butiama na mradi wa maji Bunda ambayo itanufaisha Wilaya za Butiama, Musoma na Bunda za Mkoa wa Mara. Aidha, utekelezaji wa mradi wa Miji 28 unatarajiwa kuanza katika mwaka huu wa fedha ambapo Wilaya za Serengeti, Tarime na Rorya zitanufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza miradi mingine 72 katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara. Kukamilika kwa miradi yote kutaboresha huduma ya maji kufikia lengo la asilimia 85 vijijini na asilimia 95 mijini ifikapo 2025.