Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Kituo cha afya cha Chamwino Ikulu kinahudumia zaidi ya Kata 20 za Wilaya ya Chamwino na wanawake na watoto wa kata hizo wanategemea sana huduma za kituo hicho, lakini hakina vifaa tiba muhimu kama vile ultra sound:- Je, ni lini Serikali itanunua ultra sound kwa ajili ya kituo hicho?

Supplementary Question 1

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya yetu ya Kondoa haina ultra sound na kuna Kata zaidi ya 30, lakini wanawake wanapopata shida, wanaletwa Dodoma Mjini. Kituo cha Afya cha Chamwino lkulu, kiko katika geti la Ikulu pale Chamwino hakina ultra sound, na wanawake wanatoka kilometa 50, 80, 90 wakija Dodoma Mjini,kwa ajili ya matibabu.
Je, Serikali iko tayari sasa kuongea na Bima ya Afya ili tupate mkopo huo wa shilingi milioni 72 kwa haraka?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Serikali iko tayari kuisaidia Hospitali ya Kondoa, ambayo pia haina kifaa tiba hicho; na wanawake wengi wa Kondoa, wanabebwa kilometa 150 kuja Dodoma Mjini kwa ajili ya ultra sound. Je, wako tayari kuisaidia hospitali hii ya Kondoa wakapata kifaa hicho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tarehe 24 Februari katika ziara yangu katika Wilaya ya Chamwino niliweza kufika Chamwino soko la Bwigiri na kuangalia ujenzi wa Halmashauri ya Chamwino. Nilipofika pale kweli nilitembelea majengo yote na kuangalia kituo cha afya kile kikoje, na kwakweli na mimi sikuridhika, ndiyo maana nikatoa maelekezo siku ile ile, kwamba kinachotakiwa sasa tuangalie jinsi gani kituo kile kitapata ultra sound. Na bahati mbaya wakati ule bajeti ilikuwa haijaanza, na niliwaelekeza kwamba ikiwezekana waangalie kupitia mfuko wa Bima ya Afya, hali kadhalika katika mpango wao wa bajeti. Lakini kwa bahati mbaya kutokana na ukomo wa bajeti walishindwa kungiza katika bajeti yao.
Mheshimia Naibu Spika, lakini hata hivyo katika maagizo yangu niliyoyatoa nimshukuru sana DMO wa Chamwino na timu yake ya Mkurugenzi kwamba waliweza kufanya utaratibu wa kuwahusisha wenzetu wa NHIF. Na mchakato huu upo mbioni na mimi nina imani kwamba ombi lako Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari, ni kwamba tulishakuwa tayari ndiyo maana nikaagiza. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa ni kuendelea kupambana ili wenzetu wa NHIF waweze kusaidia Kituo cha Afya Chamwino.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la Kondoa; ni kweli kutoka Kondoa mpaka hapa ni mbali; na pale ultra sound hakuna, kama Serikali tumeliona hili. Lakini vilevile naomba nisisitize jambo hili jamani; kwamba mambo haya wakati mwingine yote lazima yaanze katika mchakato wetu wa bajeti. Kama bajeti katika vipaumbele inawezekana hatukuweka ultra sound inaonekana kwamba sisi wenyewe tumedhulumu vityo hivyo. Kwa hiyo, jukumu langu kubwa mimi ni kuwasisitiza ndugu zangu Wabunge, tunapoweka katika mchkato wa bajeti tuangalie kipi kipaumbele cha zaidi? Tupunguze yale mambo mengine ambayo hayana maana tuweke katika sehemu ambayo moja kwa moja tunaenda kumsaidia mama na mtoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama Serikali tumelisikia hili na kwamba tutawahusisha wenzetu wa NHIF ili kama itawezekana waangalie ni jinsi gani waipe kipaumbele Hospitali ya Kondoa. Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kuwa Mheshimiwa Mbunge yuko makini katika hili, najua tutashirikiana na wenzetu wa NHIF. Na siku ile alizungumza pale katika Hospitali yetu ya General, wenzetu watalisikia hili watatupa kipaumbele pale Kondoa.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

Kituo cha afya cha Chamwino Ikulu kinahudumia zaidi ya Kata 20 za Wilaya ya Chamwino na wanawake na watoto wa kata hizo wanategemea sana huduma za kituo hicho, lakini hakina vifaa tiba muhimu kama vile ultra sound:- Je, ni lini Serikali itanunua ultra sound kwa ajili ya kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Matatizo yaliyopo kwenye Kituo cha Afya cha Chamwino ni sawa sawa na matatizo yaliyopo kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ambayo inahudumia takribani wananchi zaidi ya 500,000, hawana kifaa cha ultra sound. Ningependa kujua sasa ni lini Serikali itaona kuna umuhimu wa dhati kabisa wa kuleta huduma hii ya kifaa cha ultra sound kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ili kuondoa hizi adha kwa wananchi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimemsikia Mheshimiwa Esther, lakini katika jibu langu la msingi alishasikia pale awali. Mimi naamini kwamba ni kweli changamoto hii ni kubwa na ndiyo maana katika mwaka huu ukiangalia katika bajeti yetu ya TAMISEMI, development budget karibuni ni shilingi bilioni 182.5.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hiyo kuna sehemu zingine watu wameweka vipaumbele vya vifaa tiba, wengine wameweka magari ya wagonjwa, wengine wameweka miundombinu kujenga wodi za wazazi. Kwahiyo, japokuwa hii ni changamoto iliyopo pale Tarime naomba vilevile Waheshimiwa Wabunge tutumie fursa zinazowezekana katika mchakato wa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ni kwamba mchakato wa bajeti wa mwaka huu ulivyokuja Wabunge wengi sana tulikuwa katika vikao vingine vya Kamati, inawezekana hiyo ndio ndo ikawa miongoni mwa changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini huko mbeleni tunapokwenda tuangalie jinsi gani tufanye ili michakato ya bajeti itakavyoendelea sisi Wabunge tuwe mbele kuwa main stakeholders katika ile budget process. Hii itasaidia vile vipaumbele ambavyo sisi kama Wabunge wa majimbo tunaona kwamba ni jambo la msingi kuwa katika bajeti yetu viweze kufanyiwa kazi.
Hata hivyo Mheshimiwa Esther Matiko nimelisikia jambo hili, tutawaambia wadau mbalimbali kuona ni jinsi gani wanaweza wakatusaidia. Lengo letu kubwa ni kwamba mwananchi katika kila angle katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aweze kupata huduma bora na mama aweze kunusurika katika suala zima la uzazi.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Kituo cha afya cha Chamwino Ikulu kinahudumia zaidi ya Kata 20 za Wilaya ya Chamwino na wanawake na watoto wa kata hizo wanategemea sana huduma za kituo hicho, lakini hakina vifaa tiba muhimu kama vile ultra sound:- Je, ni lini Serikali itanunua ultra sound kwa ajili ya kituo hicho?

Supplementary Question 3

kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa ukosefu wa vifaa tiba katika Wilaya ya Chamwino ni sawasawa kabisa na ukosefu vifaa tiba uliopo katika Wilaya ya Kasulu. Wilaya ya Kasulu haina ultra sound, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea Wilaya ya Kasulu haina vifaa-tiba vya kupimia sukari (test strips), na hili linasababisha wagonjwa kuweza kupoteza maisha kwa sababu wanapopima vipimo kinakosekana kipimo cha sukari wakati mwingine wanaweza kupoteza maisha kwa sababu wanapima…
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo. Sasa ni lini Serikali itahakikisha inapeleka ultra sound Kasulu lakini sambamba na vifaa vya kupimia sukari? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Gezabuke, Mbunge Viti Maaalum kutoka Mkoa wa Kigoma, ambaye amerudi tena baada ya wananchi kumpa ridhaa kama ifauatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kigoma kuna changamoto hiyo kama alivyosema Mbunge. Lakini jibu langu lile litakuwa vilevile kama jibu la awali. Mkoa wa Kigoma ni Mkoa ambao upo pembezoni zaidi, kwa hiyo hata kufanya ile referral system ni changamoto kubwa sana. Sisi kama Serikali naomba tuseme kwamba eneo la Mkoa wa Kigoma tutalipa kipaumbele maalum katika kipindi hiki na naomba nikwambie kwamba jukumu langu kubwa baada ya Bunge la Bajeti miongoni mwa mikoa ambayo natarajia kuitembelea ni Mkoa wa Kigoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu kubwa tutakalolifanya ni kuwahimiza watu katika suala zima la ukusanyaji wa mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba tutakapokusanya mapato vizuri, kama nilivyoelekeza katika maeneo mablimbali, kwamba tukitumia mifumo ya electronic zile collection zetu zitakuwa kubwa, na zitatuwezesha kununua vifaa tiba. Lakini kwa Mkoa wa Kigoma kuwa Mkoa wa pembezoni kama Serikali tutaupa kipaumbele. Mheshimiwa Genzabuke kwa sababu wewe ni mwakilishi wa wakina mama na watoto, naomba nikwambie kwamba tumesikia lakini tutaangalia jinsi ya kufanya ili Kigoma ipewe kipaumbele cha msingi. (Makofi)