Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 32 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 258 2016-05-30

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Kituo cha afya cha Chamwino Ikulu kinahudumia zaidi ya Kata 20 za Wilaya ya Chamwino na wanawake na watoto wa kata hizo wanategemea sana huduma za kituo hicho, lakini hakina vifaa tiba muhimu kama vile ultra sound:-
Je, ni lini Serikali itanunua ultra sound kwa ajili ya kituo hicho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Aloyce Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kituo cha afya cha Chamwino hakina ultra sound kwa ajili ya huduma za mama na wajawazito na watoto. Kifaa hicho kinagharimu shilingi milioni 72.0 ambazo hazijawekwa kwenye bajeti ya Halmashauri kutokana na ukomo wa bajeti. Hata hivyo Halmashauri imewasilisha maombi ya mkopo wa shilingi milioni 72 katika Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kupata fedha zitakazowezesha kifaa hicho kununuliwa, katika Bajeti ya mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, wagonjwa wanao hitaji huduma hiyo kwa sasa, wanapewa Rufaa kwenda katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, ambapo huduma hiyo inapatikana.