Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya matukio ya moto katika Masoko kwenye maeneo mbalimbali nchini?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa matukio haya ya kuungua masoko yamekuwa yakitokea kwa masoko haya ambayo hayajajengwa kisasa kwa sababu ya ukosefu wa miundombinu hiyo ya uzimaji wa moto na kwa kuwa Serikali wamekuwa wakichukua kodi au tozo katika haya masoko kwa sababu kuna wafanyabiashara humo.

Je, sasa Serikali haioni ni muhimu kufikiria namna ya kuwalipa fidia wale wananchi ambao waliumizwa na matukio haya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa hayo masoko ya zamani hayana miundombinu, je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa-train vijana miongoni mwao wanaofanya biashara na kuwawezesha wawe na vifaa vyote ili inapotokea majanga haya basi iwe ni raihisi wao wenyewe waweze…

SPIKA: Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Paresso, kama ifuatavyo: -

Mhehimiwa Spika, kuhusu suala la kulipa fidia hili ni suala la kisheria kwa mujibu wa sheria tulizonazo, sasa hatuwezi kusema lolote kwa sababu Bunge lako halijatoa utaratibu kama huo. Hata hivyo, nadhani lililo la umuhimu ni elimu ya kinga dhidi ya majanga haya ili yasitokee kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la mafunzo hilo ni jambo jema na tumeanza kutoa kupitia kwa Scout, lakini vilevile na mifumo yetu ya Serikali za Mitaa ili kuwawezesha watu hawa kujikinga na majanga ya moto au kuzima yanapotokea katika hatua za awali. Nashukuru.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya matukio ya moto katika Masoko kwenye maeneo mbalimbali nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Manispaa ya Moshi kumekuwa na matukio mengi sana ya kuungua masoko, lakini jambo la kusikitisha ni kwamba manispaa haina ya magari ya kutosha ya kuzimia moto tunategemea magari kutoka TPC. Hivyo basi husababisha mali za wananchi kupotea. Je, ni lini Serikali itanunua magari ya kuzimia moto katika Manispaa ya Moshi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuena Bushiri kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Bushiri amekuwa akifuatilia kwa karibu masuala ya Kilimanjaro kuhusiana na Zimamoto, Polisi na mambo yote yaliyo chini Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mhehimiwa Spika, tunafahamu kama tulivyosema katika hotuba yetu iliyosomwa na Waziri wiki iliyopita maeneo mengi yana changamoto ya magari, lakini katika bajeti ijayo tumetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari, tutayapeleka kwenye maeneo strategic maeneo ya kimkakati ambayo yamekuwa yanakumbwa na tatizo la namna hii. Hata hivyo, uwepo wa magari tu si suluhisho la kudumu, bali utayari wa wananchi kukabiliana na mambo haya, lakini vile vile kinga dhidi ya majanga ya moto.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya matukio ya moto katika Masoko kwenye maeneo mbalimbali nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Matukio ya ujambazi, watu kupigwa, panya roads kwenye maeneo ya Kawe, Kunduchi na maeneo mengine yamezidi sana. Sasa ni nini tamko la Serikali?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali ya nyongeza la Mheshimiwa Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze kwa namna anavyofuatilia suala hili, kuna wakati ameongea kwenye YouTube tumeona, lakini baadhi ya taarifa hazikuwa kweli sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ujambazi nakupigwa ni ni jukumu la msingi la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na hususani Jeshi la Polisi. Nadhani mmemsikia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, IGP na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Tumeahidi kushughulika na vijana hawa, tumesema wakitu-beep sisi tutawapigia. Kwa hiyo, kwa tahadhali hiyo, tunaomba watafute kazi nyingine ya kufanya badala ya uhalifu wanaofanya dhidi ya binadamu kwani hatutauvumilia. Ahsante.