Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha mifumo ya upatikanaji wa tiketi kwa wasafiri wa reli ya kati?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kumekuwa na mrundikano sana wa abiria katika stesheni ya Tabora Mjini na Stesheni zinazofuata za Goweko, Tula na Malongwe wakienda pale wanakosa tiketi au tatizo la mfumo. Je, Serikali haioni haja ya kuongeza mabehewa ili wananchi wanapokwenda kupata huduma hiyo waweze kupata huduma na seat ili waweze kusafiri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumekuwa na changamoto ya mfumo wakienda pale mfumo ukiwa chini hawawezi kupata tiketi na wakipanda kwenye treni wanapigwa faini asilimia 100. Je, Serikali haioni haja ya kuboresha hii mifumo ili abiria akienda pale asipate usumbufu wa kupata tiketi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igagula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia masuala haya ya mifumo pamoja na Wabunge wote wa Mkoa wa Tabora. Hata hivyo ameomba suala zima la kuongezewa mabehewa ili kuweza kuwa na route nyingi katika kusafirisha wananchi ama abiria kutoka Tabora mpaka Dar es Salaam, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan tayari alishatoa idhini na tulishasaini mkataba wa ununuzi wa mabehewa mengine mapya 22 yenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 14, lakini pamoja na hilo tutakarabati behewa 37 ili kuongeza safari za kutoka Tabora kuja Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema changamoto za mfumo; ni kweli wakati mwingine kunakuwa kuna changamoto za mfumo kwa sababu ya internet. Nilishatoa maelekezo kwa uongozi wa TRC kwamba sasa wafikiri nje ya mfumo huu ili watumie mfumo unaoitwa USSD kwa maana ni Unstructured Supplementary Service Data ili kuweza kupatikana mfumo wakati wote, lakini hata hivyo mfumo tulionao unaruhusu kufanyakazi kwa njia ya offline mode.

Mheshimiwa Spika, nitoe maelekezo na maagizo kwa Ma- TT pamoja na wote wanaohusika na masuala ya booking clerk kwamba wahakikishe tiketi zinapatikana hata kama mfumo haupatikani kwa sababu unaruhusu mfumo wa offline mode.

Mheshimiwa Spika, ahsante.