Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 169 2022-05-10

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha mifumo ya upatikanaji wa tiketi kwa wasafiri wa reli ya kati?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha na imeanza matumizi ya mifumo ya kielektroniki kwa maeneo yote yenye huduma ya internet ikiwemo Tabora kwa ajili ya kuboresha huduma na kurahisisha upatikanaji wa tiketi mtandao kwa wananchi. Mfumo wa ukatishaji tiketi kwa maana ya e-ticketing ulizinduliwa mwezi Aprili, 2020, kwa lengo la kupunguza matumizi, kuongeza mapato na ufanisi wa Shirika pamoja na kuondoa mianya ya upotevu.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, Serikali inaendelea na jitihada za kuongeza vitendea kazi kwa maana ya injini na mabehewa kwa lengo la kuboresha huduma kwa kuhudumia wananchi wengi zaidi. Tayari pia imesaini mkataba wa ununuzi wa mabehewa 22 ya abiria na vipuri kwa ajili ya ukarabati wa mabehewa 37 ya abiria. Aidha, kuongezeka kwa vitendea kazi hivi kutaongeza idadi ya safari za treni za abiria na hivyo kupunguza changamoto ya upatikanaji wa tiketi kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, ahsante.