Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nilikuwa nataka commitment ya Serikali ni lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nilikuwa nauliza kwa kuwa sasa hivi mfumo ndiyo unaochagua wapi nyumba ziende. Kwanini sasa Wizara isipeleke hizi nyumba kwa majimbo badala ya mfumo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Jimbo la Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali imeshaweka commitment ya kwa kutenga fedha katika bajeti yake, na ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha ambao tumepitisha bajeti ya TAMISEMI, tumetenga jumla ya bilioni 81.48 ambazo zitatumikwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika shule za misingi na sekondari.

Kwa hiyo, ni commitment kubwa ya Serikali. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba tutafanya hivyo katika maeneo yote nchi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, ni kwamba amekuja tu mfumo kwamba tupeleke katika majimbo. Niseme tutaendelea kuzingatia maeneo yote yenye uhitaji mkubwa ikiwemo katika jimbo lake kama ambavyo ameainisha. Kwa sababu lengo la Serikali ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba tunamaliza hii kero kwa kadri fedha itakavyokuwa inapatikana. Ahsante sana.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Longido ina changamoto kubwa sana ya nyumba za walimu ambayo inasababisha ukosefu mkubwa wa walimu katika wilaya hii. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi kwamba fedha tumetenga kwa mwaka huu unaokuja lakini vile vile tutazingatia maeneo ya pembezoni ikiwemo Longido kama ambavyo ameainisha. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Chemba ina jumla ya shule za msingi 103 za Serikali na tumeongeza shule nane kwa matokeo ya fedha za UVIKO, lakini asilimia 70 ya shule zote hizi zipo vijijini ambavyo ni ngumu sana kupata nyumba za kupanga, naomba kujua mna mkakati gani wa maksudi wa kujenga nyumba za Walimu kwenye shule hizo? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Monni Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkakati wa Serikali ni kujenga nyumba maeneo ya pembezoni na miongoni mwa mikakati ambayo nimeainisha ni pamoja na kutenga fedha, vilevile tuna miradi mbalimbali ambayo tumeiainisha ikiwemo BUST, EP4R, EQUIP 2 yote hii lengo lake ni kuhakikisha kwamba tunapunguza hiyo adha kwa hiyo tutazingatia maeneo hayo ikiwemo Jimbo la Chemba. Ahsante. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, Ahsante. Sambamba na nyumba za Walimu Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga ofisi za Walimu au kukarabati ofisi zilizopo kwa ajili ya Walimu na kuweka samani zake ndani ya ofisi hizi, hasa katika Jimbo letu la Temeke? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave Mbunge wa Temeke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama tulivyojibu kwenye upande wa nyumba za Walimu sasa hivi moja ya mkakati wetu mkubwa ni kuhakikisha kila tunapokenga madarasa tunaweka na ofisi za Walimu, kwa hiyo huo ndio mkakati wa Serikali ili kuhakikisha kwamba walimu wanakuwa na maeneo mazuri ya kukaa ambayo yatawasaidia katika utendaji wao wa kazi wa kila siku. Hivyo, hilo lipo na limezingatiwa na Serikali ya Awamu ya Sita. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Hili linahusu Majimbo yote ya Vijijini hasa hasa kule ambako kumejengwa shule shikizi, nyumba nyingi za Walimu zilizopo zimejengwa kwenye maeneo ambayo angalau Mwalimu anaweza akapata nyumba za kupanga, sasa hizi shule ambazo ziko kwenye maeneo ambayo Mwalimu hapati hata nyumba za kupanga.

Je, kwa nini hizo shilingi bilioni 43 zisielekezwe kwenye maeneo kama hayo badala ya kuangalia maeneo mengine? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa George Kakunda Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana nilipokuwa najibu swali nimeainisha kwamba maeneo ambayo tutayazingatia zaidi ni maeneo yenye uhaba, maeneo ya pembezoni kwa hiyo ni moja ya jambo ambalo sisi tumelizingatia. Ahsante sana.