Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 162 2022-05-10

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya mahitaji ya Nyumba za Walimu Nchini.

Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo, Serikali itaendelea kupeleka fedha kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu kulingana na upatikanaji wa fedha kupitia vyanzo mbali mbali.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 37.85 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika shule za Sekondari na shilingi bilioni
43.63 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika Shule za Msingi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya nyumba za walimu katika maeneo ambayo kunauhitaji mkubwa likiwemo na jimbo la Segerea kadri fedha zitakavyopatikana.