Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo kwa makundi ya vijana na wanawake wanaopata mikopo ili waweze kujiwezesha kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali la nyongeza.

Katika vikundi hivyo 6317 kwa upande wa Zanzibar ni vingapi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Jimbo la Bububu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana kwa kazi nzuri kubwa anayoifanya, lakini naomba niichukue hili ili tukafanye mchanganuo kuona kwa upande wa Zanzibar vilikuwa vikundi vingapi kati ya hivi vilivyoainishwa.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo kwa makundi ya vijana na wanawake wanaopata mikopo ili waweze kujiwezesha kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Wengi wanaochukua mikopo hiyo ni pamoja na kinamama ambao wanakuwa na vikundi vyao vya vikoba, lakini hela zao huwa zinazunguka kwenye makasiki na wakati mwingine kasiki linaibiwa.

Ni lini sasa Serikali itazungumza na mabenki ili waweze kuongezewa angalau asilimia moja ya kuweka kwenye account zao kuendesha viofisi vidogo dogo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba akina mama na vikundi vingine na hususani akina mama wanakopa lakini pia wana shughuli za vikoba, na kuna risk hizo za mara nyingine kupoteza fedha kwa njia mbalimbali. Nimepokea wazo lake, tumepokea kama Serikali tutalifanyia tathmini kuona namna ya kuongea na benki ili tuone njia sahihi ambayo inaweza kufanyika kunusuru changamoto.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo kwa makundi ya vijana na wanawake wanaopata mikopo ili waweze kujiwezesha kiuchumi?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsane kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha vile vikundi vya wanawake na vijana ambao wanapata mikopo ili mikopo hiyo isipotee wafanyiwe tathmini ya kazi wanazokwenda kuzifanya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Hokororo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya vikundi hivi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu havijapewa mikopo, moja ya kigezo muhimu ni kufanya tathmini ya uwezo lakini na utayari wao wa kuanza kufanya shughuli hizo za ujasiliamali ili kuhakikisha zile fedha wanazokopeshwa zinaleta tija, lakini pia hazipotei. Tumeendelea kufanya hivyo na ndiyo maana tumeona matokeo mazuri ya urejeshaji ukiangalia kwa miaka inavyokwenda mpaka sasa kuna improvement kubwa na tutaendelea kufanya hivyo.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo kwa makundi ya vijana na wanawake wanaopata mikopo ili waweze kujiwezesha kiuchumi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa vikundi vingi ambavyo vinapata mkopo wengi wanatoka maeneo ya mijini. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba elimu inatolewa ili wanawake na vijana wa vijijini pembezoni waweze kupata mkopo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika halmashauri zetu zote zikiwemo za vijijini kuna fungu ambalo linatengwa kupitia maafisa maendeleo ya jamii kwa ajili ya kuhamasisha, kuelimisha, wanawake vijana na watu wenye ulemavu kunufaika na fursa za mikopo hiyo. Kwa hiyo suala hilo tunalifanya na jambo kubwa ambalo tunaendelea kulifanya ni kuongeza nguvu ili wananchi wapate nguvu ya kutosha waweze kunufaika na mikopo hiyo.