Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 163 2022-05-10

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo kwa makundi ya vijana na wanawake wanaopata mikopo ili waweze kujiwezesha kiuchumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma Mbunge wa Jimbo la Bububu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 23 ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu pamoja na marekebisho yake, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimeelekezwa kutenga fedha kutoka katika fedha za marejesho ya mikopo hiyo kwa ajili ya kuwajengea uwezo pamoja na ufuatiliaji wa shughuli za vikundi kwa vikundi vilivyokubaliwa kupata mikopo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya vikundi 6,317 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika halmashauri zote nchini vimepatiwa mafunzo kuhusu masuala ya uongozi, usimamizi wa fedha, uendeshaji wa miradi na utoaji wa taarifa.