Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kilomita 50 za barabara ya Mugakorongo kuanzia mpaka wa Uganda na Tanzania utaanza ili kuvutia biashara na watalii?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza na nishukuru kwa hatua ambazo Serikali imefikia kwa ujenzi wa barabara hii. Pia naomba kujua barabara ya Murushaka kwenda mpaka Murongo, ambayo walishatangaza tender, wamefikia wapi, ili barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Swali la pili; tunayo barabara inayotoka Kyerwa, Makao Makuu ya Wilaya, Nyakatuntu, Kamuli, Kitwe, Mabira mpaka inaunganisha Karagwe; nataka kujua, barabara hii ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wetu na ndiyo kuna uzalishaji mkubwa, lakini imekuwa ikijengwa kwa kiwango ambacho siyo kizuri: Ni lini Serikali itaweka barabara hii yote iweze kujengwa kwa changarawe ipitike wakati wote? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Omurushaka – Nkwenda - Kyerwa hadi Murongo itaanzwa kujengwa kilometa 50 kati ya Kyerwa kuja Omurushaka kilometa 50. Utaratibu utakaotumika ni kusanifu na kujenga. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii tayari tender ilishatangazwa na mwisho wa kupokea tender ni tarehe 10 mwezi huu wa Tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; nampongeza sana Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kwa ufuatiliaji. Kwenye suala hili alilouliza la pili, amekuja ofisini mara kadhaa; na tumekwambia kwamba baada ya kutoa haya maelezo, tumetoa maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera ili akaangalie barabara hiyo ili iweze kutengenezwa yote kwa kiwango cha changarawe. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kyerwa kwamba kazi hiyo itafanyika katika bajeti ya mwaka unaokuja. Ahsante. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kilomita 50 za barabara ya Mugakorongo kuanzia mpaka wa Uganda na Tanzania utaanza ili kuvutia biashara na watalii?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya Namanyere – Kirando – Kipili ni barabara ambayo ni muhimu sana kwa ajili ya kukuza uchumi wa Wilaya ya Nkasi na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla. Ningependa kujua ni lini ujenzi wa barabara hii utaanza kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara iliyotajwa ya Namanyere – Kirando – Kipili ambayo inakwenda ziwani ni barabara muhimu sana. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tulishafanya usanifu na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami barabara hii muhimu sana kwa uchumi wa Tanzania na hasa uchumi wa wana Rukwa na Jimbo hasa la Nkasi Kaskazini. Ahsante.

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kilomita 50 za barabara ya Mugakorongo kuanzia mpaka wa Uganda na Tanzania utaanza ili kuvutia biashara na watalii?

Supplementary Question 3

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nilikuwa naomba kuuliza swali: Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Mgungira – Magungumka – Ufana – Mwankalaja kwenda Kaugeri, Mlandara hadi Mwaru? Kwa maana barabara hii imejengwa madaraja kwa kipindi cha miaka 12, mpaka leo madaraja haya hayajakamilika kwa maana ya kujengewa tuta.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili TANROADS waweze kukamilisha ujenzi wa barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kingu, Mbunge wa Singida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba tu Mheshimiwa Kingu tuweze kuonana. Kama barabara imejengwa kwa miaka 12 na haijakamilika, tuweze kuona changamoto ni nini? Nitakuomba Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuweze kukaa tuone nini cha kufanya kuikamilisha hii barabara muhimu sana kwa Wana-Singida lakini pia wananchi wa Jimbo lako. Ahsante sana. (Makofi)