Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 160 2022-05-09

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa kilomita 50 za barabara ya Mugakorongo kuanzia mpaka wa Uganda na Tanzania utaanza ili kuvutia biashara na watalii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara ya Omugakorongo – Kigarama hadi Murongo yenye urefu wa kilometa 110.1 utatekelezwa kwa awamu. Awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa sehemu ya barabara kutoka Murongo hadi Businde eneo la Kigarama yenye urefu wa kilometa 50. Ujenzi wa sehemu hii utaanza Murongo na pia utahusisha ujenzi wa Daraja la Murongo lililopo mpakani mwa Tanzania na Uganda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.