Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA - K.n.y MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Magu?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa sababu Serikali inao mpango wa kutafuta fedha na kuhakikisha vyuo hivi vinajengwa. Wilaya ya Magu imeshatenga zaidi ya hekari 30, ikitegemea Serikali ipeleke fedha kwenye eneo hili na wananchi waweze kufaidika na vyuo hivi vya VETA. Sasa Serikali tunaomba commitment yake kwamba itakapopata fedha, Wilaya ya Magu iwe ya kwanza kwa sababu hata kule Kwimba, wanajenga kituo ambacho kina miaka miwili leo na hakijakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, pamoja na Serikali kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka kwenye ujenzi wa vyuo vingi vya VETA, vyuo vingi vimekuwa havina vifaa vya kufundishia na matokeo yake wanafunzi wengi wanajifunza kwa theory peke yake.

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kila Chuo cha VETA kinapoanzishwa kilichopo kinakuwa na vifaa vyote stahiki kwa ajili ya kufundishia. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mabula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwennyekiti, ni kweli katika sera yetu ya Serikali kwamba tutakwenda kujenga Chuo cha VETA katika kila Wilaya na Mkoa katika Taifa letu. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na kumpongeza vilevile kwa ufuatiliaji wa karibu, iwapo Serikali itapata fedha, basi kipaumbele cha kwanza kitakuwa katika Wilaya hiyo ya Magu na Wilaya nyingine ambazo tayari zimeshatenga maeneo kwa ajili ujenzi wa vyuo hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimtoe wasiwasi vilevile katika eneo hili la pili la vifaa. Kama anavyofahamu Mheshimiwa Mbunge katika awamu ya kwanza tunakwenda kujenga Vyuo 25 katika Wilaya 25 mbalimbali nchini, tayari Vyuo hivyo viko mwishoni kabisa katika kumalizika kwake na tunaamini ifikapo Julai, vyuo hivi vinaweza kuanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hili Serikali tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya vyuo hivi ili basi vitakapofunguliwa pamoja na ufundishaji wa nadharia lakini ufundishaji wa vitendo uwe umepewa kipaumbele zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi tayari Serikali inafanyia kazi jambo hili na fedha tayari imeshatengwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia. (Makofi)

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA - K.n.y MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Magu?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi wanayofanya ya kuhamasisha VETA katika nchi yetu.

Nataka kufahamu tu kwa ufupi ni lini Serikali inakwenda kutekeleza ujenzi wa VETA pale Mufindi, ikizingatiwa kwamba sasa tarehe 29 Aprili, Baraza la Madiwani limeamua VETA ikajengwe Nyololo, lini utekelezaji wake unafanyika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Kihenzile, alikuwa anafuatilia suala hili kwa karibu. Mheshimiwa Kihenzile wewe mwenyewe ni shahidi nadhani tumeshawahi kuonana siyo mara moja, siyo mara mbili na umeshawahi kuja ofisi zaidi ya mara moja kwa ajili ya suala hili. Kwa vile tayari mmeshapitisha kwenye Baraza lenu la Madiwani ambalo ndilo lenye mamlaka ya kupanga wapi chuo hiki kijengwe. Nikuondoe wasiwasi iwapo Serikali itapata fedha, kipaumbele kitakuwepo katika maeneo haya ya Mufindi kwa sababu tunajua kule kuna shughuli nyingi sana ambazo zinahitaji masuala haya ya ufundi kuweza kuzingitiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nikuondoe wasiwasi nalo hili tunalifahamu tutalitilia mkazo kwa karibu zaidi. Ninakushukuru sana. (Makofi)