Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 154 2022-05-09

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA - K.n.y MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Magu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Bonivetura Destery Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kuwezesha upatikanaji wa fursa za ujuzi na stadi mbalimbali za maisha kupitia elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi katika Mikoa na Wilaya zote nchini. Kutokana na nia hiyo, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa Vyuo vya VETA kwa awamu katika Mikoa na Wilaya mbalimbali ikiwemo Wilaya ya Magu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi ambacho Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya ya Magu na maeneo mengine, wananchi wa Magu wanashauriwa kutumia Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma cha Mkoa wa Mwanza pamoja na Vyuo vingine vya VETA na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vilivyopo jirani kwa ajili ya kupata elimu na mafunzo ya ufundi. Ninakushukuru sana.