Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yanatia moyo kwa wana Kilindi na Watanzania kwa ujumla. Ninayo maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa Jimbo la Kilindi lina eneo kubwa la utawala; lina vijiji 102, tarafa nne, kata 21 na vitongoji 611, na gari ambalo linatumika sasa hivi ni gari bovu sana. Je, Serikali iko tayari kutuongezea gari lingine baada ya utaratibu huu ambao upo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa utaratibu huu ambao kila Mbunge anaujua hapa kwamba kila halmashauri itapata magari ya wagonjwa kwa mpango wa COVID-19. Je, ni lini utaratibu huo utakamilika ili wananchi wa Tanzania waweze kupata magari hayo? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omar Mohamed Kigua, Mbunge wa Jimbo la Kilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianza kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Omari Kigua kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwasemea wananchi wa Jimbo la Kilindi. Mimi nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais – TAMISEMI, tutaendelea kushirikiana naye ili kuhakikisha wananchi wa Kilindi wanapata maendeleo wanayoyatarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ukubwa wa eneo na uhitaji wa gari jingine, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika magari haya yanayonunuliwa, jumla ya magari yote yanayonunuliwa kwa ajili ya huduma za afya katika halmashauri zetu zote, ni magari 407. Kwa hiyo tuna magari 195 kwa ajili ya wagonjwa lakini tuna magari 212 kwa ajili ya ajili ya huduma za usimamizi, chanjo na mambo mengine yanayohusiana na afya. Kwa hiyo, kila halmashauri itakuwa na magari mawili.

Mheeshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie kwamba kutakuwa na magari hayo mapya na ni kabla ya Juni mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuhusiana na lini magari hayo yanakuja, taratibu za manunuzi zinaendelea na mpango wa Serikali ni kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Juni, magari yawe yamepatikana; au kama atachelewa sana basi ni Julai, lazima magari yatakuwa yamefika kwenye halmashauri zetu, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi ya swali la nyongeza. Niipongeze sana Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa mpango wake huu wa kununua magari ya wagonjwa katika halmashauri zetu zote nchini, hongera Serikali. Nikiamini pia kwamba Hospitali yangu ya Wilaya ya Kinyonga, pale Kilwa Kivinje tutapata gari hili. Lakini tuna changamoto kubwa ya vituo vyetu vya afya ambavyo havina magari haya ikiwemo Kituo cha Afya Nanjilinji. Je, kwa upendelea wa pekee Ofisi ya Rais- TAMISEMI itapeleka gari ya wagonjwa Nanjilinji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Comrade Ally Kassinge Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Ally Kasinge, kwa kweli anapambana sana kuwasemea wananchi wa Jimbo lake la Kilwa, na sisi tunamhakikishia tutaendelea kuhakikisha tunampa ushirikiano ili wananchi wa Kilwa wapate matunda ya Serikali yao ya Awamu ya Sita. Nimhakikishie, kwamba tunafahamu kwamba Kilwa, nayo itapata gari la wagonjwa, itapata gari la usimamizi, lakini kituo cha Nanjili nakifahamu kiko mbali lakini kinahudumia wananchi wengi. Na katika magari 195 tuna halmashauri 184. Kwa hiyo, tutafanya tathmini na kuona uwezekano wa kuongeza gari Kituo cha Afya Nanjilinji. Ahsante.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi ya kuuliza swali; na hili swali naliuliza kwa mara ya pili, na ninamuuliza Mheshimiwa Waziri huyu huyu aliyesimama hapa. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Same, ina majimbo mawali; na majimbo mawili haya yameketi kwenye asilimia 40 ya Mkoa wa Kilimanjaro. Hospitali ya Wilaya iko Magharibi ambako ni mbali sana na Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wakifariki huku Mashariki wanapelekwa Mkoa wa Tanga kwa sababu kituo cha afya ni kimoja na hakijakamilika na hakuna hata mortuary mpaka sasa hivi na bado hatuna hata gari la wagonjwa. Mheshimiwa Waziri leo nijibu vizuri nielewe hivi mtaliangalia lini Jimbo langu la Same Mashariki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza sana sana Mheshimiwa Anne Kilango Malecela kwa uchapa kazi wake ambao umekuwa mfano hapa Bungeni, na wananchi wa Same Mashariki wana mwakilishi bora kabisa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge uliuliza wiki iliyopita swali hili na leo umeuliza na Serikali hii ni Sikivu, tumepokea tutafanya tathmini tutahakikisha kituo cha afya hicho kinaletewa gari la wagonjwa ili wananchi wapate huduma bora za afya, ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi, Wilaya ya Tanganyika ina tarafa tatu na umbali wa tarafa moja hadi nyingine ni zaidi ya kilomita 130, na jiografia yake ni mbaya. Nilikuwa naomba kuuliza Serikali ni lini itaongeza gari la wagonjwa kwenye tarafa ya Kalema, Kabungu na Mwesi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ni wilaya kubwa lakini hizi tarafa ambazo amezitaja na nyingine zinahitaji kupata upendeleo wa makusudi kupata gari la wagonjwa. Niseme kwa ujumla, Waheshimiwa Wabunge wote tutafanya tathmini, tunafahamu jiografia ya halmashauri zetu na majimbo zinatofautiana, tutafanya tathmini kwa maeneo ambayo ni makubwa yanahitaji magari zaidi ya moja. Hivyo, kati ya yale magari yanayoongezeka tutapeleka ikiwemo tathmini ya Tanganyika. Ahsante.