Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 151 2022-05-09

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya wagojwa katika Wilaya ya Kilindi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua Mbunge wa Kilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Kilindi ina gari mmoja la kubebea wagonjwa lililopo kwenye Kituo cha Afya Songe ambalo hutumika kubeba Wagonjwa kwenye Vituo vya Kutolea Huduma za Afya. Uwepo wa gari hilo hautoshelezi kukidhi mahitaji ya halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO 19 itanunua magari 195 ya kubebea wagonjwa ambapo kila Halmashauri itapata gari moja, ikiwemo Halmahsauri ya Kilindi. Ununuzi wa magari haya utaboresha hali ya utoaji huduma za afya kote nchini. Ahsante.