Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kukarabati Shule za Msingi za Nansimo, Kenkombyo, Kitengule na Namibu zilizopo katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza Serikali kwa majibu yake mazuri na program ambayo imeitoa. Ila nina swali moja dogo la nyongeza. Kwa vile wahenga walisema seeing is believing, je, Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili, uko tayari tuongozane, mguu kwa mguu twende tukatembelee hizo shule ambazo nimezitaja ili uone jinsi ambavyo zimechakaa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo tayari kwenda na Mheshimiwa Mbunge hata kabla ya Bunge kwisha, ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kukarabati Shule za Msingi za Nansimo, Kenkombyo, Kitengule na Namibu zilizopo katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa shule kongwe zinajumlisha pia shule ya Zombo, shule ya msingi pale Jimbo la Mikumi pamoja na Kidodi. Je, Serikali haioni wakati umefika sasa wa kuona namna bora ya kuboresha shule hizi kwa kuzikarabati.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mpango ambao tunao sasa hivi miongoni mwa shule ambazo zitafanyiwa ukarabati ni pamoja na hizi ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziainisha.