Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 150 2022-05-09

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kukarabati Shule za Msingi za Nansimo, Kenkombyo, Kitengule na Namibu zilizopo katika Jimbo la Mwibara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Shule 2,147 shule za msingi kongwe nchini ambazo zilianzishwa kabla ya kupata Uhuru mwaka 1961. Hali ya miundombinu ya shule hizo ni mseto zikiwemo zenye hali nzuri na nyingine zenye miundombinu chakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais-TAMISEMI imeanza kufanya tathimini ya hali ya miundombinu ya shule zote za msingi kupitia mradi wa BOOST ili kubaini mahitaji ya ujenzi wa miundombinu mipya ya shule na hali ya uchakavu wa miundombinu iliyopo. Tathimini hiyo imeanza mwezi Aprili, 2022 na itakamilika mwezi Julai, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo ya tathimini hiyo yatatumika kuandaa mpango wa uendelezaji na ukarabati wa miundomibinu ya Shule za Msingi kwa miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi mwaka 2025/2026 zikiwemo Shule za Msingi Nansimo, Kenkombyo, Kitengule na Namibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kufanya ukarabati wa miundombinu ya shule kongwe za msingi kadri fedha zitakapopatikana.