Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nami niulize maswali mawili ya nyongeza. Nkasi hatuna shida na uwajibikaji wako Mheshimiwa Waziri, changamoto ni kwamba kwa kuwa umetambua kwamba tuna Ziwa Tanganyika lakini bado hatuna maji kwa hiyo hatuna shida na chanzo. Ni lini utaonyesha uthubutu kuepusha fedha ambazo zinatumika kwenye usanifu na bado miradi haijakamilika lini utakamilisha huo mradi wa maji ili na sisi watu wa Nkasi tuweze kupata maji ya uhakika?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili kwa kuwa Mheshimiwa Waziri mwenyewe alifika Nkasi mwaka jana na akatoa fedha, ukawaambia kwamba mwezi Desemba mradi huo utakamilika wa maji lakini mpaka leo nazungumza hizo Kata Tano za pale Mjini hazina maji. Ni lini sasa mtaachana na hizi fikra za kutumia visima badala ya kuelekeza nguvu zote ili kusaidia sasa Mkoa mzima badala ya Wilaya ya Nkasi peke yake? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Aida, kwa kweli nimefika Nkasi na unafanya kazi kubwa unafanya kazi nzuri. Kubwa Mwenyezi Mungu hawezi kukupa fursa ya Ziwa halafu akakupa fursa ya kuchimba visima. Maeneo mengi ambayo yamekuwa na Maziwa mengi ukichimba visima tunafeli. Kwa hiyo, namna pekee ya kuhakikisha tunatatua tatizo la maji eneo la Rukwa ni kuhakikisha tunatumia Ziwa Tanganyika na kazi hiyo imekwishaanza.

Mheshimiwa Spika, kubwa nimuombe Mheshimiwa Mbunge aendelee kutupa ushirikiano na Wizara ya Maji hatutomuacha katika Jimbo lake la Nkasi kuhakikisha wananchi wale wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo la pili tulifika katika mradi ule wa Namanyele, Mkandarasi alikuwa anadai kiasi cha fedha na fedha tumeshampa sasa wananchi wanapata huduma ya maji. Kikubwa ni kuongeza sasa usambazaji ili wananchi wa eneo lile waendelee kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tuko tayari na tutashirikiana bega kwa bega katika kuhakikisha wananchi wake katika eneo la Namanyele wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri Mkoa wa Mbeya una vyanzo vingi sana vya maji lakini chanzo kikubwa tunaliona Ziwa Nyasa ni kama linaweza likatatua tatizo la maji.

Ni lini Serikali mtaweka fedha pale ili Wilaya zote Saba ziweze kupata maji kwa kupitia Ziwa Nyasa? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mbunge nikushukuru sana. Tunatambua kabisa katika eneo la Mbeya kumekuwa na ongezeko kubwa pamoja na uwekezaji wa miradi ya maji. Tumepata ombi maalum la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini...

SPIKA: Mheshimiwa Waziri mbona hapo kama umepunguza sauti au mimi ndiyo sijakusikia. (Kicheko)

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba nirudie kwamba tumepata ombi maalum la Mheshimiwa Mbunge wa Jiji la Mbeya Mheshimiwa Spika kwamba tukitumia chanzo cha Mto Kiwira tunakwenda kumaliza kabisa tatizo la maji. Kazi hiyo tumeshapata Mhandisi Mshauri na tumeshasaini mkataba Mheshimiwa Spika nataka nikuhakikishie sisi ni Wizara ya Maji si Wizara ya Ukame. Tutahakikisha ndoto ile ambayo umeilenga tunaenda kuitekeleza na wananchi wa Jiji la Mbeya wapate huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nami kunipa nafasi niulize swali moja kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, katika moja ya safari zake ambazo Mheshimiwa Waziri alifanya Mkoani Rukwa alifika Kalambo na akafika Ziwa Tanganyika eneo la Kasanga na alijionea jinsi ambavyo tuna utajiri mkubwa sana wa maji. Sasa katika majibu yake sijamsikia katika utafiti ambao unaendelea kama na chanzo kile cha kutoka Kasanga nacho ataki-consider ili kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Mkoa wa Rukwa kwa ujumla, Songwe na ikiwezekana hata Mbeya maana maji ni mengi sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kauli ya Mheshimiwa Waziri.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru sana lakini nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge. Kwa kweli nilifanya ziara na akanipa ombi maalum la kwenda kunionesha eneo lile, nikushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, tumefanya ugunduzi mkubwa sana na nimwombe sasa tuwaachie wataalam, lakini bila kuwaachia tu wataalam na sisi tuendelee kutoa mawazo yetu ni namna gani sasa rasilimali ile toshelevu tuliyonayo iende kunufaisha Kalambo na maeneo mbalimbali mengi ili katika kuhakikisha tunatatua matatizo ya maji, ahsante sana.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo hili ambalo liko Nkasi na sawa na tatizo ambalo liko Biharamulo hasa tukitegemea kwamba tuna mradi mkubwa wa kutoa maji Ziwa Victoria kuyaleta katika Mji wa Biharamulo.

Ni nini sasa kauli ya Serikali kuhusu utekelezaji wa mradi huo katika mwaka huu wa fedha? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Engineer Ezra, kwa kazi kazi kubwa nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Biharamulo.

Mheshimiwa Spika, namna ya kutatua tatizo la maji Biharamulo ni kuhakikisha tunaanzisha mradi mkubwa wa kutumia Ziwa Victoria na tumeanza jitihada katika maeneo mbalimbali. Nimwombe awe mvumilivu, nadhani kipindi ambacho tutaisoma bajeti yetu tarehe 12 mambo yatakuwa bambam, tuko pamoja. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 5

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mwezi mmoja uliopita nilisoma kwenye vyombo vya Habari kwamba vyombo vya ADB imepitisha zaidi ya bilioni 250 kwa ajili ya Bwawa la Farkwa. Sasa nataka kujua ni lini mradi huo utaanza? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana juu ya ujenzi huo wa mradi huo wa Bwawa la Farkwa. Utekelezaji wa miradi ya maji inategemea na fedha na hapa, nitumie nafasi hii kumpongeza sana nakumshukuru Mheshimiwa Rais kwa jitihada zake mahususi kabisa, African Development Bank bodi yake imeridhia sasa kutupatia fedha ya kuhakikisha ujenzi wa bwawa lile unatekelezeka. Kwa hiyo, suala la mikopo lina taratibu zake, lakini kikubwa tutaliharakisha ili kuhakikisha mradi ule unaenda kuanza na wananchi wa Farukwa kwa maana ya Jimbo lake la Chemba na wananchi wa Jiji la Dodoma waende kupata huduma ya maji safi na salama.