Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 133 2022-05-05

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Wilaya ya Nkasi kutoka Ziwa Tanganyika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kutumia Maziwa Makuu kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi waishio karibu na vyanzo hivyo ikiwemo wananchi wa Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali imeanza kutumia Ziwa Tanganyika kuwanufaisha wananchi wa Wilaya ya Nkasi ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imekamilisha miradi ya maji ya Kirando, Kamwanda, Mkinga na mradi wa maji Kabwe.

Kukamilika kwa miradi hiyo kumeboresha hali ya upatikanaji wa huduma maji Wilayani Nkasi kutoka asilimia 47 hadi asilimia 53.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali itaendelea na usanifu wa miradi ya maji kupitia chanzo cha Ziwa Tanganyika kwenye vijiji 10 vya Kilambo, Kala na Tundu Kata ya Kala, Izinga, Mwinza na Wampembe Kata ya Wampembe, Ninde, Kisambala na Namasi Kata ya Ninde na Mandakerenge Kata ya Kipili. Vilevile, katika mwaka 2022/2023, usanifu utafanyika kwa ajili ya kupeleka maji Mji wa Namanyere pamoja na vijiji vilivyoko kilomita 12 kila upande ambapo bomba kuu litapita. Usanifu huo unatarajiwa kukamilika katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023 na baadaye ujenzi utaendelea.