Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na ahsante kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali.

Je, Mheshimiwa Waziri unatuhakikishia pamoja na usanifu huo wa kutoa maji Ziwa Tanganyika kuleta katika Mkoa wetu wa Katavi. Je, usanifu huo utaambatana pamoja na ufungaji wa mita za uhakika ambazo zitaenda kuondoa tatizo la ubambikizwaji wa bili kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi? Ahsante.(Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Dada yangu Martha kwa kazi kubwa anayoifanya katika Mkoa wa Katavi, kwa kweli ni kielelezo chema kwa ajili ya kuwapigania wananchi wa Katavi kupata maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie kwamba tumepewa maelekezo mahsusi na Mheshimiwa Rais kuhakikisha tunatumia rasilimali toshelevu kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. Nimhakikishie kwamba tunapokwenda katika bajeti hii 2022/2023 na asubiri katika bajeti yetu ya Wizara yetu ya Maji tumejipanga katika kuhakikisha tunakwenda kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika ili wananchi wa Katavi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, pili ni juu ya suala zima la malalamiko ya bili za maji. Wizara ya Maji tumeendelea kufanya mageuzi makubwa sana na hata katika wiki yetu ya maji tumeshaanza kuweka mifumo katika kudhibiti, pia katika kuhakikisha tunamaliza tatizo hili la maji kabisa la bili, tumeona kabisa kizuri huigwa tunaona sasa ni muda wa kutumia teknolojia zilizopo kwa kuanzisha prepaid meter kwa maana ya mita za maji (LUKU) ili kuhakikisha kwamba tunaondokana na tatizo la hili la maji.

Mheshimiwa Spika, tumesharuhusu wadau mbalimbali wameshaweza kufunga ili kuweza ku-study na muda si mrefu tutatoa maelekezo kwa ajili ya uanzaji wa hizo mita za maji(LUKU). Ahsante sana.(Makofi)

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Je, Serikali itakuja lini na mpango wa kusambaza maji katika vijiji vya Wilaya za Mkoa wa Mara zinazozunguka Ziwa Victoria ukizingatia tayari vyanzo vya maji viko wazi kutokana na Ziwa Victoria na vijiji vingi havina maji? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Dada yangu Agnes Marwa na atakubaliana na mimi Wizara ya Maji tumewekeza miradi mikubwa sana katika Mkoa wa Mara. Tuna mradi wa Mugangu, Kyabakari Butiama, zaidi ya Bilioni 70. Pia tuna mradi pale Bunda ambao umekwishakamilika kwa ajili ya chanzo.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie kila ambapo bomba kuu litakapokuwa linapita vijiji jirani tutahakikisha vinapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi napenda niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Jimbo la Kwimba, Misungwi, Ilemela, Sengerema na Nyamagana?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Serikali imeendelea kujitahidi na inaendelea kuwekeza kuhakikisha kwamba tunakarabati na kujenga miundombinu mipya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama. Mathalani kwa eneo la Misungwi tumeshakwenda na Mheshimiwa Rais na tumekwishazindua mradi mkubwa wa zaidi ya Bilioni 12 katika kuhakikisha wananchi wale wanapata huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. THEA M. NTALA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami napenda kuuliza Lake Nyasa ina maji ya kutosha sana. Serikali ina mpango gani wa kutumia yale maji angalau vijiji vile karibu na lake vipate maji ya kutosha? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na pia nikubaliane nae. Sisi kama nchi hapa palipofikia hatuna sababu tena ya kulalamika juu ya changamoto ya maji, lazima tukubali tutumie rasilimali toshelevu tulizonazo ambazo Mwenyezi Mungu ametujalia katika kuhakikisha tunawekeza miradi mikubwa na kutatua matatizo ya maji.

Mheshimiwa Spika, tumeona jitihada za Mheshimiwa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan juu ya uwekezaji wa miradi mikubwa tunataka kuyatoa maji ya Ziwa Victoria kuyaleta Dodoma. Pia mpango wetu ni kuhakikisha maji ya Ziwa Tanganyika yanaenda kuwanufaisha wananchi katika eneo hilo la Mkoa wa Ruvuma. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 5

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Serikali inayo mpango wa kuleta maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria hapa Dodoma lakini ambako Ziwa Victoria lipo katika Mkoa wa Mwanza kwenye Jimbo la Sumve hakuna maji ya uhakika ya bomba kutoka Ziwa Victoria. Serikali imekuwa ikiahidi kwamba itatupelekea maji hayo kwa bajeti mbili mfululiozo.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Sumve?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na nimwambie tu kwamba baada ya dhiki sio dhiki, baada ya dhiki ni faraja. Jitihada kubwa zimefanyika katika Mkoa wa Mwanza Majimbo yote yamefikiwa na uwekezaji wa mradi wa Ziwa Victoria kasoro Jimbo la Sumve.

Mheshimiwa Spika, ni muda muafaka sasa katika bajeti yetu hii tunayokwenda nayo 2022/2023 kuhakikisha tunapeleka sasa maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo lako la Sumve.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 6

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto kubwa ya maji inayotukumba katika Mkoa wetu wa Mtwara hususan kwenye Jimbo langu la Mtwara Vijijini. Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia chanzo cha maji cha Mto Ruvuma?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, nataka niweke bayana rasilimali za maji tulizonazo juu ya ardhi na chini ya ardhi ni zaidi ya Bilioni 126. Bilioni 105 ni maji yaliyopo juu ya ardhi, kikubwa ni lazima rasilimali hizi toshelevu tulizonazo zitumike. Kwa eneo la Mto Ruvuma kwa maana ya Mtwara
tukitumia chanzo cha Mto Ruvuma tutamaliza kabisa tatizo la maji katika Mkoa wa Mtwara. Kwa hiyo, hiyo ni dhamira yetu na Serikali tuna maongezi na wadau mbalimbali naamini imani hii tunakwenda kuitekeleza na kuhakikisha wananchi wa Mtwara wanaenda kuondokanana tatizo kabisa la maji. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 7

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Naomba nifahamu ni lini Serikali itakamilisha usambazi wa maji Ziwa Basutu ambako imefikia tu eneo moja kwa sasa na maeneo yaliyotarajiwa ni 12?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, kwanza anafanya kazi kubwa nzuri na nimekwishafika katika Jimbo lake. Kikubwa ahadi ni deni, Serikali na dhamira ya Rais wetu tutahakikisha kwamba tunakwenda kuyatumia maji yale ya Ziwa Basutu na wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 8

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwa kuwa, Serikali imewekeza sana katika hii miradi ya maji vijijini na changamoto ninayoiona katika vile Vyama vya Ushirika vya maji ni kukosa mfumo mzuri wa kukusanya mapato. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia kupata drilling system itakayosadia kukusanya maji kiurahisi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza ninathamini mchango mkubwa na jitihada kubwa za uwekezaji wa miradi ya maji vijijini. Serikali kuanzisha Wakala wa Maji Vijijini katika kuhakikisha inatatua tatizo la maji vijijini. Tumeona tuna jumuiya zetu hizi za watumiaji maji, changamoto kubwa jumuiya za watumiaji maji ni katika suala zima la usimamizi. Moja tumetoa maelekezo kwamba katika kila mradi sasa kutakuwepo na Technician kupitia wananfunzi ambao wanatoka katika Chuo cha Maji. Pili, tunataka kila mradi lazima awepo Mhasibu ambaye ataweza kusimamia na kuhakikisha kwamba tunaweka mifumo.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tutatangaza mfumo rasmi wa kuhakikisha kwamba wanakuwa na bei rahisi hata vijijini ili katika kuhakikisha wanapata huduma ya maji bila ya usumbufu wowote.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 9

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Je, ni lini Serikali itatumia chanzo cha Ziwa Rukwa kulisambazia Jimbo la Momba maji ili kuondoa kadhia na changamoto ya maji ambayo tunaipata?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Kwa kweli vyanzo toshelevu ndiyo suluhu ya matatizo ya changamoto katika Majimbo mbalimbali. Kwa hiyo, mkakati wa Wizara na maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali toshelevu katika kuhakikisha kwamba tunatatua matatizo ya maji.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunajitahidi kutafuta fedha katika kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali toshelevu na wananchi wako wa Momba hatutowasahau katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. (Makofi)