Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 132 2022-05-05

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kutoa Maji Ziwa Tanganyika na kuyapeleka Mkoa wa Katavi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya huduma ya upatikanaji wa maji Mkoa wa Katavi ni asilimia 71 kwa Vijijini na asilimia 60 kwa Mjini. Katika kuboresha huduma ya maji Serikali imeanza kutekeleza miradi ya maji kwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 mradi unaoendelea kutekeleza ni Mradi wa Maji Karema katika Wilaya ya Tanganyika utakaohudumia vijiji vya Kapalamsenga na Songambele.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kutumia Maziwa Makuu kunufaisha wananchi waishio karibu na vyanzo hivyo ikiwemo wananchi wa Mkoa wa Katavi uliopo karibu na Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali itaajiri Mtaalam Mshauri wa kufanya usanifu wa kina wa ujenzi wa miundombinu wa chanzo cha maji (intake) chenye uwezo wa kuzalisha maji mengi kutoka Ziwa Tanganyika na kuwezesha wananchi wa Wilaya za Tanganyika, Mlele, Mpanda na maeneo ya karibu kunufaika na chanzo hicho.