Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Songea?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali naomba kuuliza swali la nyongeza. Hospitali ya Wilaya ya Mbinga Halmashauri ya Mbinga Mji ilijengwa mwaka 1970, na mpaka sasa hivi majengo yake yamechakaa. Sasa hivi Serikali ina mpango mkakati wa kuhakikisha hospitali hizo zilizochakaa majengo zinajengwa upya.

Je, lini Serikali itatenga fedha kuhakikisha kwamba majengo mapya yanajengwa katika hospitali ya Mji wa Mbinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunda Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya Serikali ya mwaka ujao wa fedha 2022/23 jumla ya shilingi bilioni 16 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati au ujenzi wa Hospitali za Halmashauri kongwe na chakavu, ambapo mpango ni kujenga hospitali 19. Kwa hivyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaangalia kama hospitali hiyo ipo kwenye orodha hiyo lakini kama haipo kwenye orodha hiyo tutafanya tathmini ili tuweze kuweka mpango wa kuikarabati hospitali hiyo. Ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Songea?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hospitali ya Wilaya ya Ilemela imejengwa lakini mpaka leo hatuna vifaa tiba.

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Ilemela?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba hospitali zetu zote za halmashauri mpya ambazo zimekamilika ujenzi wake zinanunuliwa vifaa tiba ili zianze kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa. Na katika bajetii ya mwaka huu ambao tunamaliza Juni 30, Serikali ilitenga shilingi bilioni 33.5, na fedha zote Mheshimiwa Rais amezipeleka Bohari Kuu ya Madawa (MSD) na tayari taratibu za manunuzi zinaendelea kwa ajili ya vifaa tiba.

Mheshimiwa Spika, pia katika mwaka ujao wa fedha, fedha zimetengwa bilioni 69.95 kwa ajili ya vifaa tiba. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Hospitali ya Wilaya ya Ilemela ni kipaumbele.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Songea?

Supplementary Question 3

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Hospitali ya Wilaya ya Tunduru majengo yake ni machakavu kweli kweli; na mingoni mwa hospitali kongwe ile naweza kusema ni namba moja.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutujengea hospitali mpya kama sio kukarabati hospitali ile?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Tunduru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ameendelea kuwasemea kwa dhati kabisa wananchi wa Jimbo la Tunduru, na amekuja Ofisi ya Rais - TAMISEMI mara kadhaa kwa ajili ya kuomba ukarabati au ujenzi wa hospitali hii. Na mimi na yeye tumeongea mara kadhaa. Nimhakikishie kwamba kwenye bajeti hii ya 2022/2023 tutaona uwezekano wa kuingiza hospitali hiyo. Na kama tutashindwa kufanya hivyo basi tutafanya kwenye mwaka ujao wa fedha. Ahsante sana.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Songea?

Supplementary Question 4

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Mkoani Rukwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe
Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali kupitia Wizara ya Afya ni kuhakikisha mikoa yetu yote inakuwa na hospitali za rufaa za mikoa za kisasa na zenye vifaa tiba. Ninafahamu Hospitali ya Mkoa wa Rukwa ni ya siku nyingi, hivyo, Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirkiana na Wizara ya Afya tutaona mpango wa kuhakikisha inajengwa hospitali au kukarabatiwa ili iweze kuwa na sifa ambazo zinafanana na hospitali ya rufaa ya mkoa. Ahante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Songea?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Mji wa Bunda imepokea kwa mikono mikubwa uhamasishaji wa Serikali wa ujenzi wa hospitali ili kusogeza huduma ya afya kwa wananchi. Najua wametenga milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali mpya ya halmashauri kwenye Kata ya Bunda Stoo. Je, Serikali kwa mwaka huu wa fedha mko tayari kuwatengea fedha ili wananchi wa Bunda waweze kukamilisha hospitali yao ya mji ambayo iko kwenye Kata ya Bunda Stoo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali inaendelea kujenga hospitali za halmashauri ikiwemo katika Halmashauri ya Mji wa Bunda. Kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema, tayari Serikali imepeleka milioni 500. Mpango huu ni endelevu, nasi tutaendelea kupeleka fedha kwa awamu mpaka majengo yote yakamilike ili wananchi waendelee kupata huduma bora za afya. Ahsante.