Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa barabara hii ni ya muhimu sana kwenye utalii wa Serengeti ya Kusini na vipande vya kuanzia Karatu, Mbulu, Haydom, Sibiti mpaka Maswa vimeshafanyiwa upembuzi yakinifu na baadhi ya maeneo yameshaanza kujengwa. Lakini kipande cha kutokea Maswa – Malya – Nyambiti – Fulo havijawahi kufanyiwa upembuzi yakinifu na imekuwa ni ahadi kila mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haioni sasa kwamba kuna umuhimu wa kulichukulia jambo hili kwa ukubwa wake na kufanya upembuzi yakinifu na hatimaye kuijenga kwa lami barabara hii ili watu wa Jimbo la Sumve na Mkoa wa Mwanza na wenyewe wafaidi matunda ya utalii ambayo Serikali imeshaanza kufanya juhudi kubwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa barabara pacha ya barabara hii ni barabara inayotokea Magu kupitia Bukwimba – Ngudu – Hungumalwa; na barabara hii yenye urefu wa kilometa 71 tumekuwa kila siku tukiizungumza na Serikali katika bajeti inayoisha Juni imepanga kujenga kilometa 10 lakini hakuna dalili zozote za kuanza kujenga.

Je, nini tamko la Serikali kuhusu barabara hii ya muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Mwanza na Wilaya ya Kwimba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo ameulizia ambayo ipo kwenye swali la msingi nimesema Serikali itahakikisha kwamba kwanza tunaifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kama ambavyo imeainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo tunaitekeleza. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba kazi hiyo tutaifanya kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, barabara aliyoitaja ya Hungumalwa – Ngudu – Magu, barabara hii usanifu wa kina umeshapatikana na ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba mipango ipo na tuna hakika kwamba barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami kama ambavyo tumeainisha. Ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; barabara ya Singida – Iguguno – Mkarama – Sibiti – Meatu imejengwa kilometa 25 tu, na sote tunafahamu barabara hii ni shortcut kwa watumiaji au wasafirishaji wanaokwenda Mikoa ya Mara na Simiyu.

Sasa ni kwa nini Serikali isitafute fedha kwa udharura wake kuhakikisha kwamba hii barabara inakamilika ile sehemu iliyobaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu na ni njia fupi sana, lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga na inaendelea kutafuta fedha kuhakikisha kwamba barabara hii sasa tunaijenga na kuikamilisha. Ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kipande cha barabara ya kutoka Uvinza – Kasulu kupitia Basanza hakina lami, na mara nyingi matukio ya unyang’anyi na ujambazi hutokea katika barabara hiyo ya Uvinza – Kasulu.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja tayari imeshafanyiwa usanifu wa kina na ni barabara kuu ambayo inaunganisha barabara kutoka Mpanda – Uvinza kwenda Kasulu. Sehemu aliyokuwa anaisema ilikuwa inafanyika utekaji tuliamua kuipiga zege ili pawe rahisi kupitika, lakini mpango ni kuikamilisha barabara hii kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza naipongeza Serikali kwa ujenzi wa barabara ya Dodoma – Kondoa hadi Babati. Lakini ni lini Serikali itajenga mizani katika barabara hii ili isiharibike ndani ya muda mfupi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara ya Dodoma – Kondoa hadi Babati haina mizani, na ni kwa sababu wakati stadi inafanyika hapakuonekana kama kutakuwa na traffic kubwa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi tunafanya mipango ya kutafuta eneo kujenga mizani ili kuilinda hii barabara ikiwa ni pamoja na barabara ya kutoka hapa kwenda Iringa ambapo napo hapakuwa na lami, tayari tumeshaanza kujenga mizani. Kwa hiyo, Serikali imeshaliona hilo na tuko mbioni kujenga mizani ili kuilinda hiyo barabara. Ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa hii nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Napenda kuuliza swali kuhusu barabara ya Mlowo – Kamsamba mpaka Utambalila; barabara hii upembuzi yakinifu na usanifu wa kina vimeshakamilika, na mwaka jana nilipouliza swali kuhusu hii barabara Mheshimiwa Naibu Waziri aliniambia kwamba Serikali inatafuta fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali langu ni hili; je, Serikali bado inaendelea kutafuta fedha au mpango umeishia vipi? Kwa sababu wananchi wa Mbozi wanasubiri kwa hamu sana hii barabara.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa ustawi wa Mkoa wa Songwe. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina Serikali inatafuta fedha ili ianze kuijenga kwa kiwango cha lami barabara yote ya kutoka Mlowo hadi Kamsamba, ahsante.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, barabara ya kutoka Makete kwenda Mbeya ni barabara ya kiuchumi, na katika barabara 16 ambazo Mheshimiwa Rais alisaini zianze kujengwa moja ni barabara kutoka Makete kuelekea Mbeya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mmekuwa mkituambia mko kwenye tendering, tunaomba majibu wananchi wa Makete; ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili ifanye ukombozi wa uchumi wa wananchi wa Makete?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Makete – Kikondo kwenda Isyonje ni barabara ambayo ilipata kibali cha kutangazwa na ilitangazwa lakini ilikosa wakandarasi. Barabara hiyo imetangazwa tena na tarehe 22 mwezi uliopita ndiyo ilikuwa mwisho na sasa hivi barabara hii tuko kwenye evaluation ili tujue mkandarasi yupi atapata hiyo kazi.

Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi tuko kwenye taratibu za manunuzi, tunafanya evaluation ya tender, ahsante.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya kutoka Ilula – Mlafu – Mkalanga – Kising’a hadi Kilolo kwa sasa haipitiki kutokana na uharibufu mkubwa wa mvua.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuiagiza TANROADS kufanya marekebisho ya haraka ili barabara hii muhimu iweze kuendelea kupitika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii kumuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Iringa ahakikishe kwamba anakwenda kwenye hii barabara ndani ya siku mbili ili kwenda kufanya tathmini na kufanya marekebisho ya sehemu zote ambazo hazipitiki ili wananchi wa Kilolo waweze kuendelea kupata huduma ya barabara hii.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kilometa 73 kutoka Fulo – Nyambiti – Malya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya kutoka Kiranjeranje – Nanjilinji mpaka Ruangwa ni barabara ambayo Serikali imeahidi kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 mpaka 2025 lakini pia upembuzi wa kina umeshafanyika. Lini Serikali inakwenda kujenga barabara hii kwa manufaa ya wakazi wa maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii tumeshakamilisha usanifu wa kina, na haya ni maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya hii hatua ya kukamilisha usanifu wa kina Serikali inaendelea kutafuta fedha ili iweze kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami, ahsante.