Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishukuru Serikali kwa majibu hayo na naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mradi huu ndio utakuwa mkombozi kwa ukanda wote wa Pwani wa Wilaya ya Mkinga. Je, Serikali inataka kutuambia ni lini hasa mradi huu utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili kwa kuwa Waziri anaahidi hapa kwamba mradi huu sasa unaenda kuanza, yupo tayari kuandamana nami twende tukafanye mikutano ya kuwaaminisha wananchi hawa kwamba tatizo lao sasa linaenda kuondoka?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kaka yangu Dunstan Luka Kitandula, kwa kweli hali ya upatikanaji wa maji Mkinga yalikuwa ni changamoto kubwa sana na tumefanya jitihada kama Serikali ya kuchimba visima lakini kwa jiografia ile imekuwa ni changamoto.

Kwa hiyo, maelekezo ambayo tumepata na support ya Mheshimiwa Rais ni kuyatoa maji sasa ya Mto Zigi, Tanga na kuhakikisha tunakwenda kutatua tatizo la maji katika Jimbo la Mkinga. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Maji tumetoa maelekezo itakapofika Juni mkandarasi awepo site kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu mkubwa na historia itakumbuka wananchi wa Mkinga kwa jitihada unazozifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini juu ya kuambatana naye, mimi niko tayari kuongozana naye katika kuhakikisha tunaenda kufanya mikutano ili tuweze kuwahabarisha wananchi juu ya utekelezaji wa mradi huu mkubwa katika Jimbo la Mkinga. (Makofi)

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, changamoto ya maji katika Jimbo la Ushetu ni kubwa sana, lakini pia hata miradi iliyoanzishwa toka mwaka 2019 hasa katika Kata za Saba Sabini, Mkunze na Chambo haijakamilika.

Je, ni lini Serikali itaweza kukamilisha miradi hii ili wananchi hawa wa Ushetu waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze kaka yangu Cherehani kwa kweli ameingia muda mfupi, lakini amekuwa anawapigania watu wake na si mara moja ameshafika ofisini. Kubwa utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha, tutatoa fedha kwa Jimbo la Ushetu kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na wananchi wa Ushetu waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tunatumia sasa maji ya Ziwa Victoria kuhakikisha wananchi wa Ushetu wanaenda kupata maji ya uhakika. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, tunamshukuru sana Waziri kwamba tumepata mradi wa maji katika Kata ya Mabogini. Lakini baada ya manunuzi ya vifaa havijatosha kufikisha maji Umasaini eneo la Remiti. Je, Serikali ina mpango gani wa kutusaidia?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya, lakini kikubwa nataka nimhakikishie maeneo yote ambayo panaishi watu na wanahitaji maji Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imetoa maelekezo kuhakikisha tunawafikishia maji na wananchi waweze kupata huduma hii muhimu sana ya maji.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa miji 28 ulikuwa ni mradi mkombozi sana kwenye majimbo ambayo hatujawahi kuona maji ya bomba, kila nikiuliza mnaahidi mwezi mmoja unaniambia nini ili wananchi wangu wapate faraja ya maji ya miji 28?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, lakini nataka nimtie moyo ukiona giza linatanda ujue kumekucha. Taratibu zote zinazohusiana na manunuzi ya mradi wa miji 28 zimekwishakamilika na kabla ya Bunge la Bajeti ya Wizara yetu ya Maji tutakaa na Waheshimiwa Wabunge tukubaliane lini tunakwenda kusaini mradi ule taratibu zote tumeshakamilisha tunaenda kwenye signing ya mradi, ahsante sana.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tukipata ahadi ya Serikali kupitia Waziri Aweso kuanza kwa mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria kutoka Busega, Bariadi, Itilima, Maswa na Meatu. Lakini mpaka sasa haujaanza na tuliahidiwa kwamba ungeanza mwezi wa nane mwaka jana. Nini commitment ya Serikali juu ya mradi huu kuanza kwa ajili ya kunufaisha wananchi wote hao niliowataja?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, nikiri maelekezo ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan ni kutumia rasilimali toshelevu ikiwemo mito pamoja na maziwa kuhakikisha kuwa tunatatua matatizo ya maji. Tumepata fedha zaidi ya shilingi bilioni 400 kwa ajili ya kutumia Ziwa Victoria na kutatua tatizo la maji katika Mkoa wa Simiyu ikiwemo Bariadi, Busega na Itilima.

Kwa hiyo, mkakati wa Serikali sasa hivi tupo hatua ya kumpata mkandarasi na tupo hatua za mwisho. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mkandarasi atapatikana kwa wakati na utekelezaji wake tunaenda kuanza mara moja. (Makofi)

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kuniruhusu niulize swali moja la nyongeza.

Je, lini Serikali itakamilisha miradi ya maji kutoka Ziwa Victoria katika vijiji vya Mogwe, Ikongolo, Majengo, Kiwembe, Mbiti na Muswa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge pamoja na Makamu Mwenyekiti wangu wa Kamati, Serikali imefanya jitihada kubwa ya kuyatoa maji katika Ziwa Victoria na kuyaleta katika Mji wa Tabora, Igunga na Nzega. Kazi iliyobaki ni kufanya tu usambazaji.

Nataka nimhakikishie usambazi huo tutaufanya katika vijiji ambavyo amevitaja ili katika kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 7

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa wananchi wa Kata ya Isanga na Guduwe Wilaya ya Bariadi wana shida sana ya maji, muda mwingi wakina mama wanaupoteza kutafuta maji kuliko kufanya kazi za maendeleo. Ni lini Serikali itachimba visima virefu katika kata hizo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kwanza kilio cha Wanabariadi kwa maana ya Mkoa wa Simiyu kimesikika na tumepata fedha kama nilivyoeleza zaidi ya shilingi bilioni 400 katika kuhakikisha tunaenda kutekeleza mradi mkubwa. Tumefanya jitihada kubwa za kuchimba visima eneo la Mkoa wa Simiyu, lakini imekuwa ni changamoto. Kwa hiyo, solution pekee kwa ajili ya kutatua tatizo la maji Bariadi na Mkoa wa Simiyu ni kuhakikisha tunayatoa maji ya Ziwa Victoria katika kuhakikisha Wanasimiyu na Wanabariadi wanapata maji safi na salama.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 8

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, mradi wa Mhangu - Ilogi ni mradi uliochukua muda mrefu sana na mwaka jana niliuliza swali la msingi na Mheshimiwa Waziri alinipa majibu kwamba mwezi wa sita mwaka jana mradi ule ungezinduliwa. Sasa nataka kufahamu majibu ya ukweli ni lini sasa mradi huo wa Mhangu - Ilogi utakamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukimwona mtu mzima analia ujue kuna jambo. (Makofi/Kicheko)

Nimwombe Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali baada ya saa saba tukutane ofisini ili kuhakikisha kwamba hili jambo tunalikamilisha na wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 9

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri umekuwa ukiulizwa maswali ya uhitaji wa maji na Wabunge, na umekuwa ukiwapa wote ahadi za matumaini, lakini tunajua bajeti yako ni ndogo.

Sasa hudhani ni wakati sahihi wa kuliambia Bunge hili tukufu kipi kipaumbele cha Serikali kwa mwaka huu wa fedha? Kwa sababu haiwezekani kila Mbunge amesimama unampa matumaini, lakini matumaini hayatekelezwi.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Halima uliza swali lako.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, nini kipaumbele cha Serikali vijijini, mijini; maeneo gani na kwa mawanda yapi? Kuliko kupeana ahadi hapa unaanza kuulizwa tunataka utupe ahadi ya mwisho, siyo jambo jema.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimtoe hofu, wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imejipanga juu ya kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe mfano, eneo la vijijini kupitia bajeti yetu tunakwenda kutekeleza miradi 1,176 vijijini, haijawahi kutokea. Lakini pia dhamira ya Mheshimiwa Rais sasa hivi katika dola milioni 500 ambazo tumezipata, katika miji 28 tunakwenda kutatua tatizo hili la maji. Kwa hiyo, kipaumbele cha Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wa mijini na vijijini wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 10

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, naomba kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na miradi mingi sana ya maji ndani ya jimbo letu na tumekuwa tukikuomba uje uikague miradi hiyo kuona ubora wake na thamani ya fedha inayotumika.

Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri na timu yako utapata nafasi ya kuja kukagua miradi hiyo? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi Mheshimiwa Gulamali baada ya Bunge letu la Bajeti nitafanya ziara katika jimbo lake katika kuhakikisha tunasimamia na kufuatilia miradi katika Jimbo lake la Manonga. Ahsante sana.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 11

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Tukuyu una changamoto kubwa sana ya maji ikiwa ni Kata za Bulyaga, Msasani, Bagamoyo, Makandana, Ibigi, Kawetele; na Serikali iliahidi kupeleka shilingi bilioni 4.5 lakini mpaka sasa wamepeleka shilingi milioni 700 tu. Wananchi wa kule hasa akina mama wanaacha kufanya kazi kubwa za kutafuta riziki kwa ajili ya watoto wanashinda kutafuta maji.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha hizo ili kumalizia mradi huo wa maji? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua maji hayana mbadala, maji ni uhai na Serikali ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan kila mwezi tunapokea zaidi ya shilingi bilioni 14, 15 katika Mfuko wetu wa Maji.

Nataka nimhakikishie tutawapa kipaumbele Wanatukuyu ili kuhakikisha miradi yake nayo inapata fedha ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati wananchi wapate huduma ya maji.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 12

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, mimi nina swali moja tu; kuna upotevu mkubwa sana wa maji Mkoa wa Dar es Salaam hasa kwenye Jimbo la Temeke, nadhani mabomba yale ni chakavu na ya siku nyingi.

Je, mna mkakati gani sasa wa kubadilisha yale mabomba kuweka mabomba mapya ili tusipate taabu ya maji tena?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Temeke kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. Ni kweli moja ya changamoto kubwa juu ya miradi ni upotevu wa maji na tumetoa maelekezo mahususi juu ya kuhakikisha kwamba tunakarabati na kujenga miundombinu mipya ili kuhakikisha upotevu huu unakuwa katika standard.

Kwa hiyo, nataka nimhakikishie na kazi kubwa na nzuri inayofanywa na DAWASA katika kuhakikisha tunakarabati na kujenga miundombinu mipya ili upotevu huu usiendelee na wananchi wahakikishe wanapata huduma ya maji safi na salama.