Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 144 2022-05-06

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Mkinga kutoka Mto Zigi au Kinyatu utaanza kutekelezwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dunstani Luka Kitandula, Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha huduma ya maji kwa wananchi wa Wilaya ya Mkinga pamoja na maeneo ya pembezoni, Serikali imekamilisha usanifu wa mradi wa maji wa Mkinga kwa kutumia chanzo cha maji cha Mto Zigi mwezi Machi, 2022. Aidha, taratibu za kupata mkandarasi zinaendelea na anatarajiwa kuanza kazi mwezi Juni, 2022 na utekelezaji utaendelea katika mwaka wa fedha 2022/2023.