Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, Bodi za Parole za Mkoa na Kitaifa zinakaa vikao vingapi kwa mwaka na wafungwa wangapi wamepata msamaha kwa mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Serikali yanasema kwamba katika mwaka 2020/2021 ni wafungwa 70 tu waliopata msamaha kupitia Bodi za Parole. Sheria ilikuja ili kupunguza mzigo na mrundikano wa wafungwa katika magereza yetu ambapo mpaka sasa takribani wafungwa ni 15,000. Sasa ikiwa kwa mwaka tu bodi inatusaidia kusamehe wafungwa 70. Je, Serikali inaona kweli bodi ziko kazini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili matokeo haya ya kusamehe wafungwa 70 tu inawezekana kabisa ni kutokana na kwamba vikao hivi vya bodi vya kimikoa ambavyo vinakaa mara nne kwa mwaka yawezekana kabisa iko mikoa vikao hivi havikaliwi.

Je, Serikali inatoa kauli gani kuwezesha vikao hivyo viwe vinakaa mara nne kwa mwaka kama sheria inavyoelekeza?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Sheria ya Bodi za Parole iliwekwa ili kusaidia kupunguza msongamano wa wafungwa gerezani kwa kuwapa msamaha wale wanaokidhi vigezo. Nikiri kwamba kwa mwaka uliopita 2020/ 2021 vikao vingi havikukaa kwa sababu bodi ziliisha muda wake na bahati mbaya sana mapendekezo yale yalichelewa kumfikia Waziri wa Mambo ya Ndani. Lakini hivi tunavyozungumza bod izote zimeshaundwa mikoa yote, kwa hivi maelekezo yaliyotoka ni kuhakikisha kwamba vikao vinakaa kwa mujibu wa mwongozo ili wafungwa wanaokidhi vigezo waweze kunufaika na uwepo wa bodi hizi.

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, Bodi za Parole za Mkoa na Kitaifa zinakaa vikao vingapi kwa mwaka na wafungwa wangapi wamepata msamaha kwa mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mahabusu kuna wanawake ambao wanakuwa wamewekwa mle wakiwa na matatizo mbalimbali na ni wajawazito, sasa wanajifungua wakiwa bado kesi zao hazijasilikizwa.

Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha wale watoto wanaozaliwa mama zao wakiwa mahabusu hawapati changamoto za kisaikolojia mama zao wanapokuwa pale ndani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna wakati baadhi ya wafungwa wanakuwa na changamoto, wanakuwa na hali ya ujauzito na kujifungua watoto wakiwa magerezani. Upo utaratibu unaowawezesha wafungwa wa namna hii kupata huduma stahiki ikiwa ni pamoja na hao watoto wanatengwa na kupewa nafasi ya kunyonyeshwa na mama zao kama miongozo ya sekta ya afya inavyoelekeza. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge usiwe na wasiwasi juu ya watu hawa kwa sababu taratibu za kuwalinda zipo. Nakushukuru.